Meneja Masoko wa Benki ya Barclays Tanzania, Joe Bendera (kwa pili kulia), akizungumza na baadhi ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), wakati akiitambulisha program ya ‘ReadtoWork’ ya benki hiyo yenye lengo la kuwaandaa wahitimu wa vyuo vikuu na elimu ya juu kujiandaa na ajira au kujiajiri. Wengine ni baadhi ya washikiri na wawezeshaji katika mkutano huo ambao pia kituo cha televisheni cha EATV kilikuwa kikitambulisha tuzo na wasanii wanaowania tuzo hizo zinazotambuliwa na Baraza la Sanaa la Taifa.
Baadhi ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wakihudhuria mkutano huo. 
Meneja Masoko wa Benki ya Barclays Tanzania, Joe Bendera (katikati), akihojiwa na wandishi wa habari katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki wakati wa mkutano ambapo benki hiyo iliitambulisha program yake ya ‘ReadtoWork’ yenye lengo la kuwaandaa wahitimu wa vyuo vikuu na elimu ya juu kujiandaa na ajira au kujiajiri.
Meneja Masoko wa Benki ya Barclays Tanzania, Joe Bendera (kushoto), akizungumza na baadhi ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki katika mkutano ambapo benki hiyo iliitambulisha program yake ya ‘ReadtoWork’ yenye lengo la kuwaandaa wahitimu wa vyuo vikuu na elimu ya juu kujiandaa na ajira au kujiajiri.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...