Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini prof,Jamse Mdoe (wa pili kushoto) akisomo mikakati mbalimbali ya serikali wakati akifungua akifungua mkutano wa chama cha wazalishaji chumvi wadogo,kushoto ni Mwenyekiti wa Chama cha Wazalishaji Chumvi Habibu Nuru na viongozi wengine.

Na Anthony John Globu ya Jamii. 

SERIKALI imewataka wachimbaji wadogo wa chumvi kuhakikisha wanazalisha chumvi iliyo na ubora na yenye kiwango cha madini joto ilikuepuka madhara ya kiafya kwa watumiaji. 

Akizungumza leo hii Jijini Dar es salaam katika kufungua mkutano wa mwaka wa chama cha wazalashaji chumvi Naibu katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Prof, James Mdoe amesema Serikali inajitahidi kuboresha sheria za sekta ya wachimbaji wadogo na wazalishaji wa chumvi ilikuongeza uzalishaji wa mapato katika Taifa. 

Sambamba na hayo Mdoe alifafanua baadhi ya madhara ya kiafya kwa watumiaji chumvi isiyo na kiwango cha madini joto ni pamoja na kuharibu mimba na kuzaa watoto wenye ulemavu na madhara mengine ya kiafya. 

Katika uzinduzi huo wa wachimbaji wa chumvi, Prof. Mdoe alisema katika mwaka huu wa fedha 2016 hadi 2017 wizara yake itakamilisha kutengeneza kituo kimoja cha mfano wa mafunzo ya uzalishaji chumvi. Tumepanga kituo hicho kijwngwe katika wilaya ya Kilwa mkoani Lindi na kitakuwa ni kiwanda ambacho kina mchakato wote wa namna ya kuzalisha chumvi kwa ubora wa kimataifa.

Hivyo Hivyo Mwenyekiti wa chama hicho cha wachimbaji wadogo wadogo wa chumvi Habibu Nuru ameishukuru serikali kwa kuwasaidia tani 4 za madini joto pamoja na kilo miasaba zilizotolewa kwa wazalishaji hao ilikuweza kuboresha Chumvi.
Wadau mbalimbali walijitokeza kwenye mkutano huo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...