Mkurugenzi wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) ,Dk. Mwele Malecela akizungumza na waandishi wa habari katika makao makuu ya taasisi hiyo jijini Dar es salaam leo akielezea mafanikio ya Taasisi katika Mwaka 2016,katika nyanja mbalimbali ikiwmo Rasilimali na uimarishaji wa utawala Bora,Usimamizi wa utafiti za Afya,Tafiti za Afya ikinda sambamba na Matarajio yake kwa mwaka 2017
Baadhi ya Wadau na wataalamu mbalimbali pamoja na wanahabari wakimsikiliza  Mkurugenzi wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) ,Dkt. Mwele Malecela alipokuwa akitoa ufafanuzi wa mambo mbalimbali yaliyohusu mafanikio ya Taasisi hiyo katika Mwaka wa 2016 pamoja na Matarajio yake kwa mwaka 2017.Picha na Michuzi Jr.



TAASISI YA TAIFA YA UTAFITI WA MAGONJWA YA BINADAMU



TAARIFA KWA UMMA YA MAFANIKIO YA TAASISI KATIKA MWAKA 2016

Desemba 15, 2016


1.       RASILIMALI NA UIMARISHAJI WA UTAWALA BORA

Rasilimali fedha
Taasisi imeanzisha na kuanza kutumia mfumo wa fedha wa kielektroniki. Mfumo huu unaendeshwa kwa pamoja na mfumo wa serikali wa rasilimali watu. Ili kupanua matumizi ya mfumo huu mafunzo yametolewa kwa wahisbu wote wa Makao Makuu na Vituo Vikuu vya Utafiti. Lengo ni kuunganisha vituo vyote katika mfumo huo ili kurahisisha usimamizi wa mapato na matumizi ya fedha za Taasisi.

Rasilimali watu.

Taasisi imeendelea kuwapa uwezo watumishi wake katika ngazi mbalimbali za mafunzo. Watafiti 3 wameweza kuhitimu shahada za uzamivu, 6 shahada za uzamili and 4 shahada ya kwanza katika kipindi hiki.

Taasisi imeshiriki katika utoaji mafunzo kwa vitendo kwa wanafunzi kutoka vyuo vikuu vya ndani na nje ya nchi. Watafiti wa Taasisi wameshiriki kutoa mihadhara katika vyuo mbalimbali nchini – kama vile Chuo Kikuu cha Kanisa Katoliki Cha Afya na Sayansi Shirikishi, Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo, Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela. Wanafunzi kutoka vyuo vikuu mbali mbali ikiwemo Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo, Chuo Kikuu cha Dodoma na taasisi nyingine wamepata mafunzo katika maabara zetu. Pia taasisi imeendelea kuwasaidia wafanyakazi wake kupata elimu ya juu katika ngazi za astashahada, shahada ya kwanza, shahada ya uzamili na uzamivu. Watafiti watatu wametunukiwa shahada za uzamivu katika mwaka 2016.

Mwongozo wa Matumizi ya Tehama
Taasisi imeandaa Mwongozo wa Matumizi ya Tehama kwa ajili ya watumishi na wadau wake. Mwongozo huo unapatikana katika tovuti ya taasisi (http://www.nimr.or.tz)

Uandaaji wa Takwimu-msingi ya machapisho ya Taasisi
Katika kipindi cha 2016, Taasisi imeanza kuorodhesha machapisho yote ya kitaaluma iliyochapisha katika kipindi cha uhai wake (1980-2016). Takwimu-msingi hiyo itakuwa na machapisho ya majarida, vitabu na taarifa nyingine za kisayansi. Takwimu-msingi itakapokamilika, watafiti watakuwa na fursa ya kuongeza machapisho yao wenyewe kupitia tovuti ya taasisi. Hadi sana, machapisho 1,249 yamehifadhiwa kwenye takwimu-msingi.

Matumizi ya Mifumo ya Taarifa za Kijiografia
Taasisi imeendelea kujenga uwezo wa watumishi wa afya kwa ngazi za mkoa na wilaya katika matumizi ya mifumo ya taarifa za kijiografia. Jumal ya watumishi 230 kutoka mikoa 16 na wilaya 107 wamepata mafunzo hayo. Kati ya hao, 214 wametoka katika Wilaya na 16 kutoka mikoani

Huduma za Maabara inayotembea.

Taasisi imeendelea kutumia Maabara Inayotembea kutoa huduma za mafuzo katika Mkoa wa Mbeya. Lengo ni kufikisha huduma za afya karibu na wananchi. Mafunzo yalitolewa kwa njia mbalimbali, hususan kwa kutumia sinema. Magonjwa yaliyolengwa ni UKIMWI na Kifua kikuu. Katika kipindi cha Oktoba 2015 hadi Oktoba 2016, Maabara imeweza kuwafikia wateja 8,000; na asilimia 45% ya wagonjwa wa UKIMWI wameweza kuunganishwa na huduma hiyo. Huduma nyingine zinazotolewa na maabara hiyo ni kupima VVU, kupima chembechembe za damu za CD4, kupima Kifua Kikuu na saratani ya shingo ya uzazi. Huduma ya uchunguzi wa usugu wa dawa za kurefusha maisha (ARV) nayo imeongezwa katika huduma za maabara hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...