Na Amina Kibwana,Globu ya Jamii

Mtandao wa Jinsia (TGNP) imeandaa warsha ya kuchangia sera mpya ya ardhi kwa kuwashirikisha wadau mbalimbali kupitia fursa yake iliyopata kutoka Wizara ya ardhi maendeleo na makazi ili kuweza kujua namna ambavyo jinsia imeibuka katika kuchangia sera hii.

Akizungumza na Waandishi wa habari jijini dar es Salaam, Meneja Idara ya Ujenzi wa nguvu za pamoja Grace Kisetu, amesema kuwa katika warsha hiyo wameweza kuwashirikisha wadau mbalimbali kutoka katika Halmashauri wanazofanyia kazi zikiwemo Kishapu,Morogoro,Mbeya,Mara  na Shinyanga  pamoja na asasi zisizokuwa za kiserikali na wanajamii kutoka sehemu ambazo tunafanyia kazi na baadhi ya washiriki kutoka wizra ta ardhi.

“Tumeamua kuwashirikisha wadau hao ili waweze kutusikiliza na kujua chambuzi ambazo tumeweza kuzifanya ili waweze kujua ni lipi tunaloliona kwamba kwenye rasimu walioitoa pengine linahitaji kuboreshwa zaidi hususani tukiangalia je jinsia ni ninsi gani imechukuliwa na kuweza kujitokeza kwenye hiyo sera ya ardhi ya mwaka 2016”

Kwa upande wake Muwezeshaji wa warsha hiyo Magdalena Luwevangila ameongeza kuwa katika Warsha hii tunaangalia jinsi gani sera inaweza ikakidhi mahitaji ya watu wote hususan katika masuala ya kijinsia,wanawake watoto,wanaume na watu waliopo pembezoni ili iweze kufanya kazi na kumaliza migogoro ya ardhi mara tu inapojitokeza.

” migogoro ya ardhi inayojitokeza hasa kwa upande wa rushwa ambapo serikali za vijiji zimeshindwa kusimamia tatizo hili na badala yake ubadhilifu umekuwa mwingi, hivyo sera hii ijikite katika kutatua na kuondoa migogoro hiyo”.

Nae mmoja wa wadau ambaye ni Mkulima  kutoka Mkoa wa Mara Kata ya Nyakonga, Nyangi Marwa ameiomba serikali kuwaangali wanawake na wajane  waliopo pembezoni kwani wengi wao hawajui haki zao juu ya umiliki wa ardhi ili kuepuka kunyanyasaji hasa katika kipindi cha mirasi.


TGNP ni shirika ambalo lipo mstari wa mbele katika masuala ya kijinsia na imepata nafasi ya kuweza kuchangia katika suala zima la sera mpya ya ardhi , ambapo kutokana na warsha hiyo TGNP inatarajia kutengeneza kikosi kazi cha Taifa Kitakachoundwa na wadau mbalimbali ambacho kitaongeza nguvu na ufuatiliaji wa utekelezaji wa sera hizi  ili kuongeza nguvu kwenye ushawishi na utetezi wa usawa wa kijinsia hususan utekelezaji wa sera zetu .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...