|
Waziri
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim
Majaliwa(kushoto)akipokea mfano wa hundi wenye thamani ya Tsh Milioni 20 kutoka kwa Meneja wa TIB Corperate Bank Limited tawi la Arusha, Bi. Juliana
Mwansuva (kulia) ukiwa ni mchango wa benki hiyo kwa ajili ya kununua
Pikipiki ambazo Waziri Mkuu amezikabidhi leo kwenye uwanja wa Sheikh
Amri Abeid Jijini Arusha wanaoshudia kutoka kushoto ni Mkuu wa mkoa wa
Arusha,Mrisho Gambo, Mkurugenzi Mkuu wa TIB Corperate Bank, Bw. Frank
Nyabundege na Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe. |
|
Meneja
wa TIB Corperate Bank Limited tawi la Arusha,Juliana
Mwansuva(kulia)akipongezwa na Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo baada
ya kumkabidhi Waziri
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mheshimiwa Kassim
Majaliwa(kushoto) mfano wa hundi wenye thamani ya Sh 20 milioni
kwaajili ya kununua Pikipiki . |
|
Baadhi
ya walionufaika na Pikipiki zilizotolewa na Waziri Mkuu ambazo
zilichangiwa na wadau mbalimbali mkoani Arusha. Mradi huo utawawezesha
vijana kurejesha fedha zenye thamani ya Pikipiki kisha kuwa wamiliki
halali. |
|
Waziri
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim
Majaliwa na Mkuu wa mkoa wa Arusha, Me. Mrisho Gambo wakizungumza na mmoja wa
watu wenye ulemavu walionufaika na msaada wa Pikipiki leo. |
|
Pikipiki
mpya zaidi ya 200 zenye thamani ya Sh 400 milioni zilizotolewa kwa
vijana jijini Arusha leo katika ziara ya Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa. |
Imeandaliwa na www.rweyemamuinfo.blogspot.com
Arusha.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...