Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) leo imeingia makubaliano na Kampuni ya TradeMark East Africa (TMEA) ambayo itatoa msaada wenye thamani ya Dola Marekani Milioni 60 sawa na Shilingi za Kitanzania Bilioni 132 kwa ajili ya maboresho ya miradi mbalimbali ya Bandari ya Dar es Salaam.
Msaada huo unatarajiwa kusaidia uboreshaji wa barabara za ndani ya bandari, eneo la uhifadhi wa makontena, mizigo, kuongeza uwezo wa bandari kuchukua meli kubwa zaidi, kuendesha upembuzi yakinifu wa kuanisha maeneo mengine ya maboresho, kuifanya bandari ya dar es salaam kuwa rafiki ‘green port’ na kuangalia maboresho zaidi ya mifumo ya kielektroniki.
Makubaliano hayo yamefanyika leo Makao Makuu ya Mamlaka ambapo Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Eng. Deusdedit Kakoko na Mkurugenzi Mkazi wa TradeMark East Africa (TMEA), Bw. John Ulanga walitia saini makubaliano hayo mbele ya vyombo vya habari.
 Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Eng. Deusdedit Kakoko (watatu kulia) na Mkurugenzi Mkazi wa TradeMark East Africa (TMEA), Bw. John Ulanga (wapili kulia) wakiweka saini makubaliano hayo mbele ya vyombo vya habari
 Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Eng. Deusdedit Kakoko akibadilishana hati ya makubaliano na Mkurugenzi Mkazi wa TradeMark East Africa (TMEA), Bw. John Ulanga mara baada ya kuweka saini makubaliano hayo.
 Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Eng. Deusdedit Kakoko na Mkurugenzi Mkazi wa TradeMark East Africa (TMEA), Bw. John Ulanga wakionesha hati ya makubaliano mara baada ya kuweka saini makubaliano hayo.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...