Unakumbuka lile sakata la mmoja wa wagombea kiti cha Urais nchini Marekani kukumbwa na kashfa ya kutumia anwani ya barua pepe binafsi kufanya shughuli za Serikali? Au umeshawahi kuona barua pepe (Pengine unayo unaitumia) ikiwa na mchanganyiko wa herufi na namba, mfano, wateja wako watajali kweli ukiwa na barua pepe brian255@yahoo.co.tz au brian.mbunde@kampuniyako.co.tz? Sasa Extreme Web Technologies ni mshirika rasmi wa Microsoft kwa upande wa Tanzania na wanakufahamisha kwamba katika hii ulimwengu tunaoenda nao wa digitali unapokuwa na professional business email unajenga uaminifu katika biashara yako na unaonekana uko smart sana.
Pengine bado unajiuliza “Professional Email” ni nini, ukiangalia mfano hapo juu wa barua pepe ya brian.mbunde@kampuniyako.co.tz inaonesha jina kamili la mhusika na kuna domain ya kampuni. Hii inamaanisha kwamba hauwafanyi watu waone jina lingine tofauti na jina lako halisi hivyo kuwapa mitazamo tofauti linapokuja suala la biashara (Uaminifu) na hapo ndipo Microsoft O365 inakuletea kile unachohitaji mahali unapokuwa. 
Unapataje Barua pepe ya Biashara?
Jinsi ya kupata ni rahisi sana, unachotakiwa kufanya ni kuwa tu na email na kisha kuwa na “domain” ambayo imehifadhiwa mahali (server). Baada ya hapo utapewa uhifadhi kumbukumbu unaofikia 1 TB, kuwekewa Microsoft Office kwenye kompyuta mpakato yako na kwenye simu yako pia. Huduma nyingine zinahusisha “HD Video Conferencing”. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...