Na Daudi Manongi .

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu Mhe.Jenista Mhagama amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Bw. Majid Mwanga kuhakikisha ana tatua mgogoro wa  ujenzi wa barabara ya Kiwangwa-Mabohelo  yenye urefu wa kilomita 15 na kumalizika mwishoni mwa mwezi huu.

Ameyasema hayo jana Wilayani  wakati alipotembelea  miradi inayotekelezwa na Halmashauri  ya Wilaya ya Chalinze na Bagamoyo  kwa ufadhili wa Programu ya  Miundombinu ya  Masoko, Uongezaji Thamani na Huduma za Kifedha Vijijini(MIVARF)  inayosimamiwa na chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu.

“Serikali ya Awamu ya Tano ina lengo kubwa la kuwasaidia wananchi hususani wakulima ili wafikiwe na miundombinu ili kupambana na umaskini na kuboresha masuala ya masoko yao na hivyo kuwaongezea kipato”, Alisema Mhagama.

Aidha Mhe. Mhagama alisema kuwa asili ya miradi ya ufadhili wa Programu ya Miundombinu ya  Masoko, Uongezaji Thamani na Huduma za Kifedha Vijijini (MIVARF) iliyo  chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu haina fidia hivyo  anashangaa kuona ni kwanini ujenzi vipande hivyo vitatu vya barabara vinachelewa kukamilika hadi kufikia leo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,Kazi,Vijana,Ajira na Walemavu Mhe.Jenista Mhagama.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...