Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage (pichani) amesema kuwa wawekezaji na wamiliki wa viwanda wasiwe na wasiwasi kwa kuwa Tanzania ina mazingira mazuri ya uwekeza tofauti na inavyotafsiriwa na baadhi ya watu ambao wa nia ya kuwahujumu wawekezaji.
Akizungumza katika kipindi cha Mizani ya Wiki cha Azam TV, Mhe. Mwijage amefafanua kuwa serikali haina nia yoyote ya kukihujumu kiwanda cha Dangote kwa kuwa lengo la serikali ya awamu ya Tano ni kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda. Kwa kupata zaidi Usikose kuangali kipindi cha Mizani ya Wiki ifikapo saa mbili na nusu Azam Two.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...