BEN MWAIPAJA -WFM
BENKI ya Dunia
imekubali kuikopesha Tanzania fedha kwaajili ya miradi mbalimbali ya maendeleo
ukiwemo mkopo wa Dola Milioni 350 kwa ajili ya Mradi wa Upanuzi wa Bandari ya
Dar es salam.
Waziri wa Fedha na
Mipango, Dokta Philip Mpango, amewaambia waandishi wa Habari mara baada ya
kumalizika kwa Mazungumzo kati yake na Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia anaye
shughulikia Kanda ya Afrika, Mhe. Makhtar Diop, Makao Makuu ya Wizara ya Fedha
na Mipango Jijini Dar es salaam.
Amesema kuwa
kukamilika kwa upanuzi wa Babdari hiyo kutasaidia kuongeza ubora wa huduma
zinazotolewa na Bandari hiyo hatua itakayo chochea ukuaji wa uchumi wa nchi.
Kwa upande wake
Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia anayeshughulikia Kanda ya Afrika Mhe. Makhtar
Diop, amesema kuwa Benki yake imefurahishwa na hatua zinazochukuliwa na
Serikali ya awamu ya tano katika kukuza uchumi na kwamba Benki hiyo itaendelea
kushirikiana na serikali kuhakikisha kuwa malengo yaliyokusudiwa yana fikiwa
kwa haraka
Ameishauri Serikali
kuongeza ushirikiano kati yake na Sekta Binafsi katika kuchochea biashara na uwekezaji pamoja na kutupia jicho
sekta ya kilimo kwa kuboresha uzalishaji wa mazao ya kilimo na mifugo pamoja na
kuongeza thamani ya mazao hayo ili kuwawezesha wananchi wengi zaidi kuondokana
na umasikini na kuchochea uwekezaji katika sekta hiyo
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...