Nteghenjwa Hosseah, Arusha

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo ameitaka Wizara ya Mifugo, Chakula na Ushirika kuacha kutoa vibali vya kusafirisha mahindi nje ya nchi kwa wafanyabiashara wa hapa nchini kwani Serikali Mkoani Arusha ilishapiga marufuku usafirishwaji wa mahindi hayo nje ili kulinda viwanda vya hapa nchini.

Mhe. Gambo alisema hayo jana baada ya kutembelea maghala matatu ya Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula{NFRA} Kanda ya Arusha kujionea hali halisi ya uhifadhi wa mahindi katika maghala hayo na kuskiliza changamoto zake na kukuta tani 6,620 za mahindi zilizoko kwa sasa.

Alisema serikali Mkoani Arusha ilishapiga marufuku uuzwaji wa mahindi nje ya nchi lakini kuna baadhi ya wafanyabiashara wamekamatwa na vyombo vya ulizni na usalama wakiwa na vibali kutoka Wizarani vinavyowaruhusu kupeleka mahindi nchi jirani ya Kenya hali inayowafanya watendaji wa serikali kushindwa kufanya kazi kutokana na mkanganyiko huo.

Mkuu huyo alisema uamuzi wa kupiga marufuku uuzwaji mahindi nje ulitolewa na serikali kuu na Mkoa ulisimamia hilo kwa lengo la kuvilinda viwanda vya hapa nchini kwa uzalishaji wa bidhaa hivyo na kunufaika na unga na pumba za mahindi tofauti na ilivyo sasa.

Alisema kutokana na mkanganyiko huo aliwaomba watendaji wa Wizara kuacha kutoa vibali kwa wafanyabiashara kuuza mahindi nje ili kuwasaidia wenye viwanda vya nafaka kuuza unga na pumba nje wenye kiwango ili nao waweze kupata faida na nchi iweze kupata faida zaidi.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Mashaka Gambo (Pili kushoto) akiwasili katika Ofisi za Wakala wa Taifa wa Uhifadhi wa Chakula Kanda ya Kaskazini zilizoko Mkoani Arusha kuangalia na kukagua hali ya uhifadhi wa Chakula.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo(kwanza kushoto) pamoja na Meneja wa NFRA Kanda ya Kaskazini Ndg.Abdillah Nyangasa wakitembelea maghala ya kuhifadhia Chakula wakati wa ziara yake katika Ofisi hizo.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo(kwanza kulia) akikagua taarifa za mazao yaliyohifadhiwa katika Magahala ya NFRA wakati wa ziara yake ya kukagua hali ya Uhifadhi wa Chakula.
Kutoka kulia ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha Ndg. Richard Kwitega akifuatiwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo na Meneja wa NFRA Ndg. Abdillah Nyangasa wakati wa kikao na wafanyakazi wa NFRA Kanda ya Kasikazini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...