Na  Bashir  Yakub.

1.WOSIA  NININI.
Wosia  ni  matakwa  ya  mtu   ambayo  angependa  yatekelezwe  baada  ya  kifo  chake.  Yanaweza  kuwa  matakwa  kuhusu  mali, maziko, madeni, watoto,mke/wake  n.k. 

2.   AINA  ZA  WOSIA.

Tunao  wosia  wa  maandishi  na  wosia  wa  maneno,  lakini  pia  tunaweza  kupata  aina  za wosia   kutokana  na sheria  mbalimbali  zinazotumika  kugawa   mali  za  mirathi  kama  ifuatavyo :

( i )   Wosia  wa  Kiislamu. Ni  wosia  ambao  misingi  yake  itakuwa  ni  kutokana  na Quran  Tukufu, Sunna  na  Hadith  za  mtume  Muhammad S.AW.  Aina hii  ya  wosia  ni  maalum  kwa  mtu aliyeishi maisha  ya  kiislam(muislam).
( ii )    Wosia  wa  kikristo. Ni  aina  ya  wosia  ambao  misingi  yake  imejengwa  katika misingi  ya  Sheria  ya  Urithi  ya India ( The  Indian  Succession  Act ,  1865) . Sheria  hii  kwa  jina  hilo hilo  la  Sheria  ya  Urithi  ya  India  ndiyo hutumika   hapa  Tanzania kwa  mtu  aliyeishi  maisha  ya  kikiristo(mkristo). 

( iii )  Wosia  wa  kimila . Misingi  ya  wosia  huu  imejengwa  katika  Azimio  la  Sheria  za  Kimila ( The  Local  Customary  Law  Declaration Order G.N. No. 279  of 1963) .  Wosia  huu  hutumika  kwa  watu  walioshi  kimila.
3.      NI  WOSIA  UPI  UANDIKE  KATI  YA  HIZI.

Niseme  mapema  tu  kuwa  unapoandika  wosia  hakikisha unaandika  kwa  kufuata  misingi  ya  mfumo  wa  maisha  yako ( dini  yako).  Hili  si  hiari  ni  lazima.

Unapofanya  kosa  la  kuandika  wosia  bila  kufuata  misingi  ya  sheria  husika kwa  kujua  au  kutokujua   basi  wosia  huo utakuwa  ni  batili. 

Unaweza  kudhani  umeandika wosia na  kuamini  kuwa mambo  yote  sasa  yako  vizuri  lakini  kumbe hujaandika  wosia. 

4.       JE  WOSIA  NI  UTASHI  WA  MTU ?.
Ndio,  wosia  ni  utashi  wa  mtu   lakini  utashi  wenye  mipaka.  Wengi  hudhani  kwakuwa  wosia  ni  utashi  na  mali  ni  zako basi  unaweza  kufanya/kugawa    unavyotaka  .  Kwa  wanaojua  hivi  mawazo  yao  sio    sahihi. 

Pamoja  na  wosia  kuwa  utashi   ni  lazima  mgao  pamoja na  kanuni  za  uandaaji  wake  zirandane  na  sheria husika. Kama  we  ni  muislamu  lazima  ugawe  kama  sheria  na  kanuni  za  kiislamu  zinavyosema,  kama  ni  mkristo  au  mtu  wa  mila   ni  lazima  ufuate  sheria  inayokuhusu  inavyosema.  Sheria  zenyewe  ni  hizi   hapo  juu  zilizoelezwa  katika  2. 

Nirudie  tena kuwa  hautagawa  wala  kuandika   unavyotaka   isipokuwa  utagawa  na  kuandika kama  sheria  inayokuhusu inavyotaka. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...