Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO.
Hivi karibuni Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ilitangaza kufanya uchaguzi mdogo wa Ubunge pamoja na Udiwani kwa sehemu mbalimbali nchini ambazo viongozi wake wamefariki au wamepoteza sifa za kuendelea kuongoza wananchi katika sehemu husika.
Uchaguzi huo unategemewa kufanyika Januari 22 mwaka 2017 katika Jimbo la Dimani lililopo Zanzibar pamoja na Kata 20 ambazo zipo kwenye Halmashauri 19 za Tanzania Bara.
Mnamo Desemba 2016, NEC ilifanya uteuzi wa wagombea watakaogombea katika uchaguzi huo ambapo walioteuliwa kugombea Ubunge katika Jimbo la Dimani ni 11 ambao wote ni wanaume na kwa upande wa wagombea udiwani katika Kata mbalimbali za Tanzania Bara ni 71 ambapo wanaume ni 67 na wanawake ni watano.
Kwa kuangalia takwimu hizi chache tu zinatosha kutupatia majibu kuwa katika uchaguzi huu wanawake hawajajitokeza kabisa kugombea nafasi hizo wakati asilimia kubwa ya wanawake nchini wana sifa za kugombea nafasi hizo. Kwa uchaguzi huu wanawake wamewaangusha Watanzania wengi ambao wana amini kuwa wanawake wakipewa nafasi wanaweza kuzitendea haki.
Kumekuwa na wadau wengi duniani wanaotetea haki za wanawake kila kukicha kuhakikisha wanawake wanakuwa na haki sawa na wanaume kwenye nyanja mbalimbali zikiwemo za uongozi, kazi pamoja na elimu.
Pamoja na utetezi huo kushika kasi hadi kufanya jamii nzima kuamini kuwa wanawake wanaweza lakini bado wanawake wengi wanajirudisha nyuma kwa kutojiamini kama wanaweza kushika nyazfa mbalimbali za uongozi nchini.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Hivi karibuni Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ilitangaza kufanya uchaguzi mdogo wa Ubunge pamoja na Udiwani kwa sehemu mbalimbali nchini ambazo viongozi wake wamefariki au wamepoteza sifa za kuendelea kuongoza wananchi katika sehemu husika.
Uchaguzi huo unategemewa kufanyika Januari 22 mwaka 2017 katika Jimbo la Dimani lililopo Zanzibar pamoja na Kata 20 ambazo zipo kwenye Halmashauri 19 za Tanzania Bara.
Mnamo Desemba 2016, NEC ilifanya uteuzi wa wagombea watakaogombea katika uchaguzi huo ambapo walioteuliwa kugombea Ubunge katika Jimbo la Dimani ni 11 ambao wote ni wanaume na kwa upande wa wagombea udiwani katika Kata mbalimbali za Tanzania Bara ni 71 ambapo wanaume ni 67 na wanawake ni watano.
Kwa kuangalia takwimu hizi chache tu zinatosha kutupatia majibu kuwa katika uchaguzi huu wanawake hawajajitokeza kabisa kugombea nafasi hizo wakati asilimia kubwa ya wanawake nchini wana sifa za kugombea nafasi hizo. Kwa uchaguzi huu wanawake wamewaangusha Watanzania wengi ambao wana amini kuwa wanawake wakipewa nafasi wanaweza kuzitendea haki.
Kumekuwa na wadau wengi duniani wanaotetea haki za wanawake kila kukicha kuhakikisha wanawake wanakuwa na haki sawa na wanaume kwenye nyanja mbalimbali zikiwemo za uongozi, kazi pamoja na elimu.
Pamoja na utetezi huo kushika kasi hadi kufanya jamii nzima kuamini kuwa wanawake wanaweza lakini bado wanawake wengi wanajirudisha nyuma kwa kutojiamini kama wanaweza kushika nyazfa mbalimbali za uongozi nchini.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...