Na Mwandishi wetu
Muogeleaji chipukizi wa Tanzania Collins Saliboko (pichani) ambaye ataiwakilisha Tanzania katika mashindano ya Jumuiya ya Madola ya Vijana  ameahidi kuipeperusha vyema bendera ya nchi  na kuweka historia katika mashindano hayo kwa mara ya kwanza. 
Mbali ya Collins ambaye anashindana kwa upande wa wanaume, msichana Celina Itatiro ataiwakilisha nchi kwa upande wa wanawake katika mashindano hayo yaliyopangwa kufanyika nchini Bahamas kuanzia Julai 18 mpaka 23 kenye mji wa Nassau.
Collins ambaye kwa sasa anasoma Chuo cha St Felix, Uingereza, amesema kuwa ameanza mazoezi kwa ajili ya mashindano hayo chini ya kocha wake, Sue Purchase amesema kuwa amepania kufanya kile ambacho watanzania wengi hawatakitarajia kupitia mchezo wa kuogelea ambao kwa sasa unakuja juu kwa kasi.

Alisema kuwa atatumia pia mazoezi ya timu ya kuogelea ya chuo chao kama sehemu ya maandalizi, kabla ya kujiunga na kambi ya timu ya Taifa ambayo itatangazwa hapo baadaye.
“Naahidi kuitendea haki nafasi hii. Na hii inatokana na juhudi zangu katika mchezo wa kuogelea. Matokeo yangu bora ndiyo yamenipa nafasi hii. Nnaona mwanga katika mchezo wa kuogelea na ninaahidi kufanya vyema.

“Mazoezi ya hapa St Felix ni mazuri sana. Hii inatokana na kuwepo vifaa bora na walimu wazuri. Hapa pia kuna ushindani mkubwa na hivi juzi  juzi tu nilishinda nafasi ya pili kwenye mashindano ya huku Uingereza, ni matokeo mazuri na ninaahdi kufanya vyema zaidi,” alisema Collins kwa njia ya simu.

Alisema kuwa mpaka sasa ameshiriki katika mashindano mengi ya ngazi ya chuo na kupata matokeo mazuri. “Mashidano haya ya Chuo ni sehemu ya maandalizi yangu, naishi hapa chuoni, kila Napata muda mwingi wa kujifunza, Mwalimu wangu, Sue ni mkali na kwa sasa anajua jukumu langu la kitaifa, hivyo ameongeza ‘dozi’ ya mazoezi,” alisema.
Katibu Mku wa Chama Cha kuogelea Tanzania (TSA), Ramadhan Namkoveka alisema kuwa kazi iliyopo sasa ni kwa makocha kuwaandaa wachezaji katika matukio watakaoshiriki ili kuweza kufanya vizuri.
Namkoveka alisema kuwa mbali ya kusaka medali, lengo kuu la chama kwa wachezaji hao ni kupunguza muda wao ili baadae waweze kufikia muda unaotakiwa na  Shirikisho la mchezo wa kuogelea duniani, (FINA) kiwango cha muda B au A.

 Mashindano ya Jumuiya ya Madola haya yatakuwa ya sita baada ya kuanzishwa kwake mwaka 2000 ambapo  vijana 1000 wenye  umri wa miaka kuazia maika 14 hadi 18 wanatarajiwa  kushindana katika michezo mbalimbali.

 Muogeleaji wa Tanzania Celina Itatiro akichupa kwenye mashindano ya Afrika Kusini
 Collins Saliboko akichapa maji St Felix College, Uingereza
 Celina Itatiro (Mwenye kofia ya orange) akiogelea huku akiwa na kikombe cha maji kwenye paji la uso
Collins Saliboko (wa kwanza kulia) akiwa na waogeleaji wa Tanzania wanao soma St Felix College; Aliasgar Karimjee na Sonia Tumiotto mara baada ya kutwa medali katika mashindano ya chuo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...