Na. Immaculate Makilika- MAELEZO
Mawaziri 15 wa Nchi Wananchama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika ( SADC), wanatarajia kufanya mazungumzo kesho jijini Dar es salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam, Waziri wa Mambo ya nje na Ushirikiao wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga alisema kuwa mawaziri hao wanatarajiwa kuzungumza masuala mbalimbali ikiwemo elimu, ushiriki wanchi za SADC, ikiwa ni pamoja na kuzungumzia haliinayoendelea nchini Msumbiji.
“Tanzani ni mwenyeji na wenyekiti wa Mkutano huo, ambapo pia inaongoza Kitengo Maalumu cha Masuala ya Ulinzi,Usalama pamoja na Siasa, pia kamati ya siasa na diplomasia inatarajiwa kukutana pia wiki hii” alisema Waziri Mahiga
Kila mwaka mawaziri hao hukutana mara moja, kwa lengo la kuzungumzia masuala mbalimbali yanayohusu nchi wanachama wa umoja huo.Katika hatua nyingine, Waziri Mahiga alisema kuwa ,Tanzania inashirikiana na Msumbiji kufanyia kazi suala la watanzania walihamishwa nchini.
“ Hili ni zuala gumu kidogo tusitoe majibu rahisi, na hivyo Serikali zote mbili zinaendelea kufanya mazungumzo zaidi juu ya suala hili” alisema Waziri Mahiga.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...