Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO.

Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania, Simon Mwakifamba amekana kuhusika na utumaji wa ujumbe katika mitandao ya kijamii juu ya kuitisha mkutano na waandishi wa habari. 

Kauli hiyo imetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Rais wa Shirikisho hilo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari juu ya ujumbe huo uliokuwa ukisambazwa katika mitandao mbalimbali ya kijamii na kumuhusisha Rais wa Shirikisho hilo. 

Mwakifamba amesema kuwa ujumbe huo umeeleza kuwa Rais wa shirikisho hilo atakuwa na mkutano na waandishi wa habari utakaohusu wasanii waliokipigia kampeni Chama cha Mapinduzi (CCM) na kutolipwa fedha zao pamoja na kuunga mkono jitihada za msanii Wema Sepetu kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

“Kiukweli sikushiriki kwa namna yoyote katika kuuandika ujumbe huo na nimesikitishwa kuona kwamba huo ujumbe unasambazwa ukiwa na jina langu hivyo umeniletea picha mbaya kwani ni kinyume na taratibu na sheria za Shirikisho,”alisema Mwakifamba.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...