Rais Mstaafu wa
Serikali ya awamu ya pili, Alhaji Alli Hassan Mwinyi, ameipongeza Tume ya
Kikristu ya Huduma za Jamii (CSSC) kwa kutimiza miaka 25 tangu ilipoanzishwa
mwaka 1992. Akiongea katika maadhimisho
hayo, Mzee Mwinyi amesema kuwa Serikali imekuwa ikitambua na kuthamini mchango
wa makanisa na Taasisi za dini katika kuboresha huduma za Jamii.
“Nimefarijika
sana kwa kupata taarifa kuwa hadi kufikia Septemba 2016, hospitali za Kanisa 87
na vituo vya afya 45, vimeingia Mkataba na Serikali katika kutoa huduma za
afya”, alisema Rais Mstaafu Mwinyi.
Katika hatua
nyingine, Mzee Mwinyi aliongeza kuwa kwa upande wake yeye amekuwa mstari wa
mbele kwa kuwaasa ndugu jamaa na marafiki zake na Watanzania wote kwa ujumla,
kutumia huduma zitolewazo na hospitali za kanisa kwa kuwa wanatoa huduma bora,
kwa kuzingatia upendo
“ Ikiwa mnaona kazi zinawazidia na mnafikia sehemu mnanung’unika kwa kuzidiwa na kazi nyingi, basi ningesema mgomvi wenu ni mie. Maana nawaambia ndugu na Watanzania wenzangu, kuwa huduma nzuri za afya zinapatikana katika hospitali za Kanisa, kwa kuwa unahudumiwa kwa upendo pamoja na tabasamu,” aliongeza Rais Mstaafu, Mwinyi.
Rais Mstaafu Alhaji Ally Hassan Mwinyi akitembelea mabanda mbalimbali katika maadhimisho ya miaka 25 ya Tume ya Kikristu ya Huduma za Jamii (CSSC) yaliyofikia kilele siku ya tar 22/02/2017 katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam
Mkuu wa Shirika la "Pressures Blood" Tanzania Padre Chesco Msanga, akimkabidhi zawadi ya picha Rais Mstaafu Mzee Mwinyi kama kumbukumbu alipoifungua Hospital ya St. Gaspar Itigi inayoendeshwa na shirika hilo
Mzee Mwinyi akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Tume ya Kikristu ya Huduma za Jamii (CSSC).
Mzee Mwinyi akitoa Cheti kwa Profesa Costa Mahalu, moja ya watu waliyotoa msaada mkubwa wa masuala ya Sheria kipindi Tume hiyo ilipokuwa inaanzishwa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...