Afisa Mtendaji Mkuu wa Kituo cha Mpango wa uendelezaji Kilimo katika Ukanda wa Kusini mwa Tanzania (SAGCOT),Bw.Geoffrey Kirenga akiwasilisha mada kwenye Semina elekezi iliyoandaliwa na Kituo kwa Wahariri na Waandishi Waandamizi wa Vyombo mbalimbali vya Habari nchini kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kufahamu shughuli za SAGCOT katika kuendeleza kilimo na fursa zilizopo kwenye sekta ya kilimo mwishoni mwa wiki.
Mhariri wa Habari wa Gazeti la Mwananchi, Bw.Reginald Miruko akichangia mada katika Semina elekezi iliyoandaliwa na Kituo cha Mpango wa uendelezaji Kilimo katika Ukanda wa kusini mwa Tanzania(SAGCOT) kwa wahariri na waandishi waandamizi wa vyombo mbalimbali vya habari nchini kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kufahamu shughuli za SAGCOT katika kuendeleza kilimo na fursa zilizopo kwenye sekta ya kilimo.Kulia kwake Mhariri wa Biashara Gazeti la Citizen,Bw.Samuel kamndaya.
Mhariri wa habari za Biashara wa Kituo cha Channel ten,Bi.Easter Zelamula akijadiliana jambo na Afisa Mtendaji Mkuu wa Kituo cha Mpango wa Uendelezaji Kilimo katika Ukanda wa Kusini mwa Tanzania (SAGCOT),Bw.Geoffrey Kirenga mara baada ya kumalizika kwa Semina iliyoandaliwa na Kituo kwa Wahariri na Waandishi waandamizi wa vyombo mbalimbali vya habari nchini kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kufahamu shughuli za SAGCOT katika kuendeleza kilimo na fursa zilizopo kwenye sekta ya kilimo.Kushoto ni Mhariri wa Gazeti la Mtanzania, Bw.Kulwa karedia.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Kituo cha Mpango wa Uendelezaji Kilimo katika Ukanda wa kusini mwa Tanzania (SAGCOT),Bw.Geoffrey Kirenga akiwa katika picha ya pamoja na wahariri wa vyombo vya habari nchini mara baada ya kumaliza semina ya siku moja iliyolenga kutoa elimu kwa waandishi hao juu ya kazi na majukumu ya SAGCOT katika kuendeleza kilimo ili kiwe na tija kwa mkulima na Taifa kwa ujumla.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...