Na Riziki Manfred Bonzuma, Mbinga 

Wadau wa elimu na viongozi halmashauri ya Mbinga vijijini wamekutana kufanya tathimini ya elimu ikiwemo kushuka kwa ufaulu kwa wa elimu ya msingi miaka ya hivi karibuni. 

Wakizungumza katika kikao hicho ,baadhi ya wadau wa elimu wamezitaja changamoto zinazopelekea kushuka kwa elimu kuwa ni pamoja kutoboreshwa kwa masirahi ya walimu, upungufu wa walimu, ushiriki hafifu wa wazazi hususani kufuatilia maendeleo ya watoto wao na kuchangia shughuli za elimu. 

Pia wadau wameainisha changamoto zingine kuwa ni pamoja na kuto wahamisha walimu wakuu walio shushwa vyeo pamoja na kuongeza uwiano wa vitabu hasa vya kiada katika shule za halmashauri hiyo. 

Kwa upande wake mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Mbinga vijijini Gombo Samandito Gombo amesema halmashauri hiyo imejipanga kuhakikisha inaongeza ufaulu kimkoa na kitatifa hasa elimu ya msingi ambayo imeonekana kulegalega huku akiwataka walimu kuto fanya uzembe katika kufundisha ikiwemo utotoni. 

"sitakuwa na msamaha kwa walimu wanao acha kazi wanaenda kupiga boda boda ukiona nimekubaini nitakufukuza hata usiangaike kuniomba msamaha pia wapo walimu wanao kopa mpaka wanapiriliza muda wa kufundisha wanakimbia madeni waache mara moja" alisema Samandito . 

Awali katika maada za utangulizi mkuu wa Polisi wilaya ya Mbinga OCD Maganga amekemea baadhi ya wazazi kuwahusisha wanafunzi katika biashara ya dawa za kulevya na kuwataka viongozi ngazi ya vijijini na kata kutoa taarifa za wahusika wa biashara hiyo pamoja na wale wanao wapa mimba wanafunzi. 

Katika hatua nyingine mkuu wa wilaya ya Mbinga Consimas Nshenyi amendelea kukazia maagizo yaliyo tolewa wa na mkuu wa mkoa wa Ruvuma Binilith Mahenge wakati wa ziara yake wilaya Mbinga mapema mwaka huu juu ya uharibifu wa mazingira ikiwemo kufanya shughuli za kibinaadamu ndani ya mita sitini kutoka vyanzo vya maji pamoja na kuhakisha Benki tofauti zinatukamika katika kujenga majengo sio kukaa katika matanuru . 

Matokeo ya darasa la saba mwaka 2016 yanaonyesha kushuka kwa elimu katika halmashauri hiyo ya wilaya ya Mbinga baada ya kushika nafasi ya 8 katika mkoa wa Ruvuma kati ya Halamashauri 8 za mkoa huo. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...