Rais wa Marekani Donald Trump amesaini amri mpya inayozuia watu kutoka mataifa 6 yenye Waislamu wengi kuingia nchini Marekani, ikiwa ni marekebisho ya amri ya kwanza ambayo ilikwamishwa na maamuzi ya mahakama.

Amri hiyo mpya ya Rais iliyosainiwa na Donald Trump ambayo itaanza kutekelezwa tarehe 16 mwezi huu wa Machi, inashikilia marufuku ya siku 90 kwa wasafiri wanaotoka katika mataifa sita yenye waislamu wengi kuingia nchini Marekani. Nchi hizo ni Iran, Libya, Syria, Somalia, Sudan na Yemen. Inawahusu wale tu watakaotaka kupata visa kwa wakati huu, ikiwa na maana kuwa haiwaathiri watu 60,000 ambao tayari wamezipata visa, kama ilivyokuwa kwa amri ya awali.

Iraq ambayo ilikuwa kwenye orodha ya amri ya mwanzo imeondolewa, na kwa mujibu wa waziri wa mambo ya nchi za nje wa Marekani Rex Tillerson, hatua hiyo imetokana na ushirikiano uliopo baina ya nchi hizo mbili.

''Iraq ni mshirika muhimu katika vita dhidi ya kundi la IS. Mikakati ya uhakiki iliyofanywa mnamo mwezi mmoja uliopita, imeonyesha hatua mbali mbali za kiusalama, ambazo zitaziwezesha serikali ya Iraq na wizara ya mambo ya nje ya Marekani, kutimiza lengo la pamoja, la kuzuia watu wenye malengo ya kigaidi kufika nchini Marekani''. Amesema Tillerson.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...