Umoja wa Mataifa (UN) pamoja na Kamati ya Olimpiki ya Kimataifa(IOC) kwa pamoja mnamo tarehe 23 Agosti, 2013 walitiliana saini na kukubaliana kuanzishwa rasmi kwa tarehe 6 April ya kila Mwaka iwe ni SIKU YA KIMATAIFA YA MICHEZO KWA AJILI YA AMANI NA MAENDELEO. “International Day of Sport for Development and Peace” 

Chama cha Mchezo wa “Baseball/Softball” Tanzania – TaBSA, kimeamua kushiriki siku hii kwa kutoa Kombe Maalum la AMANI ambalo litashindaniwa na timu mbili zitakazojumuisha watu wa rika kuanzia miaka 15 na kuendelea bila kujali viwango vya wachezaji katika kuucheza mchezo huu wa Baseball. Mechi hiyo itakuwa katika mfumo wa Bonanza. 

Timu zitakuwa ni TIGERS na GIANTS. 

Kwa niaba ya Kamati ya Utendaji ya Chama, ninachukua fursa hii kuwaalika wote kuhudhuria na kushiriki Bonanza hili la AMANI katika viwanja vya Azania Sekondari kuanzia saa 13:30 mchana siku ya Jumamosi ya tarehe 8 April, 2017. 

Karibuni wote!. 
Alpherio Moris Nchimbi – KATIBU MKUU. 
Tumeamua kuifanya tarehe 8 April kwa kuwa tarehe 6 April ni siku ya Kazi!
Alpherio Moris Nchimbi Katibu Mkuu wa Chama cha Mchezo wa “Baseball/Softball” Tanzania – TaBSA .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...