Na  Bashir   Yakub

1.MGAWANYO  WA   WOSIA.
Wosia  umegawanyika  mara  mbili .  Upo  wosia  wa  maandishi  na  upo  wosia  wa  mdomo.  Wosia  hizi  zote  zinakubalika  alimradi  zimekidhi  vigezo  vya  kisheria  vinavyohitajika.
( a ) Wosia  wa  maandishi .  Ni wosia  ambao  unakuwa  umeandikwa. Unaandikwa  na  mtoa  wosia  na  unashudiwa  na  mashahidi. Ni  wosia  ambao  unahimizwa  sana   kwakuwa ni  wa  kuaminika zaidi.
( b ) Wosia  wa mdomo. Huu  ni  wosia  ambao  haukuandikwa  isipokuwa  aliyeutoa  alitamka  tu  kwa  maneno. Ni  wosia   unaokubalika  ikiwa utakidhi vigezo  vya  kisheria.

2.   MASHAHIDI   WANAOTAKIWA   KUSHUHUDIA   WOSIA.
( a ) WOSIA  WA   KIKIRISTO.
Sheria  inayotumika   kwa  wosia  unaoandikwa  na  mtu  aliyeishi  maisha  haya  inajulikana  kama  “The  Indian  Succession  Act  1865”. Kwa  wakristo wanaoandika  wosia  ni  sharti  kufuata  misingi  ya  sheria hii  ili  wosia  zao  kuwa  halali.
Sheria  hii  imezigawa  wosia  mara  mbili.  Kwanza  wosia  wa  upendeleo( privileged  will)  ulio  katika kifungu  cha  52   cha sheria  hiyo  na  wosia  usio  wa  upendeleo( unprivileged  will) ulio kifungu  cha  50. 
Wosia  wa upendeleo  ni  wosia  unaoruhusiwa  kutolewa  na  watu  maalum  kwa mfano  wanajeshi  wanapokuwa  vitani  na  mabaharia  wanapokuwa  baharini  huko  bahari  ya  mbali .
Wosia  usio wa  upendeleo   unawahusu  watu  wa  kawaida wasio  hao  waliotajwa. Unaitwa  wa  upendeleo  kwasababu wamepunguziwa  masharti  kutokana  na  mazingira  wanayokuwemo.
Kwa  mujibu  wa  kifungu  cha  52  wosia wa upendeleo ukiwa  wa  maandishi  sio  lazima  kuwa   na  mashahidi  au  kuwa  na  sahihi  ya  mtoa  wosia. Maandishi  tu  yasiyo  na  mashahidi  yanakubalika  na  ndio  maana  unaitwa  wa  upendeleo. Na kama  ukiwa  wa  mdomo  basi  mashahidi  wawili  wanahitajika  ili  ukubalike. 
Kwa  wosia  Usio  wa  upendeleo  unaotumiwa na  watu  wa  kawaida  mashahidi  wanaohitajika  ni watu  wawili  au  zaidi  kwa  mujibu  wa  kifungu  cha  50. Mtu  mmoja  hakubaliki  kuwa  shahidi.   Mashahidi  hawa  hutakiwa  kumshuhudia  mtoa  wosia  akisaini  wosia.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...