Na Bashir Yakub

1.KUNYIMWA  MTOTO.

Wako  watu  ni  wazazi  na  wamezaa  lakini  wameyimwa  watoto.  Zipo  sababu  nyingi  zinazopelekea  hili. Matukio  ya  namna  hii  hayawatokei  sana  wanawake  na badala  yake  wanaume  ndio  waathirika  zaidi katika hili .  Ni  rahisi  na  kawaida  mno mwanaume  kuambiwa  na  mzazi  mwenzake   kuwa  huyu   mtoto  si  wako  hata   kama   anajua kabisa  huyo  mwanaume  ndiye  mzazi  halisi .  Leo haya  sio  maajabu  tena.
Upo  usemi  wao  kuwa mwanamke   ndiye anayejua  baba  wa  mtoto. Sitaki  kueleza  ukweli  au  upotoshi  wa  usemi huu bali  nawaza  iwapo  ni  sawa  kutumia usemi  huu   kupora  haki  ya  uzazi   wa mtu  ambaye  unajua  kabisa  ndiye  mzazi  halisi.
Na kwa  bahati  mbaya  wanaokutwa  na  kadhia  hii wamekuwa  hawajui  ni  hatua  zipi  wachukue. Wapo  wanaoamua kufanya  vurugu, wapo  wanaojiua, wapo  wanaoamua  kumuachia  mola, na  wengine  hukimbilia  serikali  za  mitaa  ikiwa  ni  pamoja  na  hatua  nyinginezo  zisizofaa.
Ukweli  ni  kuwa  hatua  hizo  haziwezi  kukusaidia  zaidi  utapoteza  muda  mwingi,  gharama  na  pengine  kuzua  matatizo  mengine  ambayo  hayakuwako.  

Basi  sasa  yafaa   ujue  kuwa  sheria  imetambua  jambo  hili  na  imeweka  taratibu  nzuri  za  kufuata  ili  kuondoa  ujeuri  wa  aina  hii.
 Sheria Namba  21, Sheria  ya  Mtoto  ya  mwaka  2009  imeeleza  nini  ufanye  kama  tutakavyoona   hapa  chini.  Lakini  kabla  ya  hilo  hebu  kwa  kutaja tu  tuone  sababu  kadhaa  zinazofanya  wazazi  hasa  wa  kike kuwanyima  wazazi  wenzao  haki  ya kutambulika  kama  wazazi  wenzao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...