Mhe. Dkt Harrison Mwakyembe, Waziri wa Mambo ya Katiba na Sheria na Mbunge wa Kyela , ameshudia zoezi la kuingizwa majini kwa Meli mpya ya pili ya mizigo iitwayo MV Ruvuma kwenye bandari ya Itungi, Wilayani Kyela. 

Tukio hilo la kuiingiza Meli hiyo making limefanyika Machi Mosi . Meli hiyo yenye uwezo wa kubeba mzigo zaidi ya tani 1000 inaungana na Meli nyingine mpya MV Njombe yenye uwezo wa kubeba zaidi ya tani 1000 ambayo iliingizwa majini siku tano zilizopita. Meli zote mbili zipo kwenye hatua ya mwisho ya utengenezaji na majaribio kabla hazijaanza rasmi kubeba mizigo kwenye ziwa Nyasa. 

Tayari wateja mbalimbali wamejitokeza kutaka mizigo yao ianze kubebwa yakiwemo makampuni yanayojishughulisha na biashara ya makaa ya mawe.
 


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...