Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii
Msanii wa Bongo Movie , Vicent Kigosi 'Ray' kesho anatarajia kuzindua filamu yake mpya,itakayojulikana kwa jina la Gate Keeper katika ukumbi wa Sinema wa Quality Centre.
Ray ambaye hajatoa filamu kwa kipindi cha zaidi ya mwaka mmoja,amesema kuwa filamu hiyo ni moja ya akzi zenye ubora wa hali ya juu katika soko la filamu ambazo azijawahi kutokea tangu aanze kazi hiyo.
ametaja kuwa watu ambao ameshirikiana nao katika filamu hiyo ni Kajala Masanja, Single Mtambalike na Nicole Franklin .
Amesema kuwa filamu hiyo imeandaliwa na Rj Production na kusimamiwa na kampuni ya Steps Entertiment,aidha ametaja kuwa kingilio katika uzinduzi huo ni shilingi 10000 kwakila mtu atakaye fika katika ukumbi huo wa Suncrest Cineplex Cinema.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...