Na Bakari Madjeshi,Globu ya Jamii

Taasisi ya Sekta Binafsi nchini (TPSF) imekutana na wadau wake kujadili utekelezaji wa Soko la pamoja la Jumuiya ya Afrika  Mashariki (Common Market Protocol 2010)  tangu ilipoanzishwa upya mwaka 2010.

Wanachama wa Jumuiya hiyo walingia makubaliano ya pamoja ili kuongeza utengamano ambao ulilenga zaidi kuongeza uhuru wa watu kupita nchi za Afrika Mashariki, Kuongeza uhuru wa kusafirisha Mizigo na Biashara pamoja Uhuru wa Mitaji (Free Movement of Capital).

Akizungumza na Waandishi wa Habari katika majadiliano hayo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Sera – Taasisi ya Sekta Binafsi, Gilead Teri amesema kuwa wamekutana kufanya tathmini kujua changamoto pamoja na uboreshaji katika soko hilo.

Amesema wamekutana kujadili  ili baadae kutoa maoni kwa Serikali pamoja na viongozi wa Jumuiya hiyo, pia ni jinsi gani Tanzania inaweza kunufaika zaidi na soko la pamoja.

Katika soko hilo Tanzania inanufaika zaidi kupata Kodi,Wananchi kupata ajira kutokana na soko kubwa, familia kupata kipato pamoja na kukua kwa Teknolojia ya uzalishaji.
 
 Sehemu ya Wadau wa Taasisi ya Sekta Binafsi wakifuatilia mada iliyokuwa ikiwasilishwa na Mkurugenzi wa Sera wa TPSF, Gilead Teri.
 Mkurugenzi wa Sera – Taasisi ya Sekta Binafsi, Gilead Teri akizungumza na baadhi ya wadau wa Taasisi hiyo juu ya kujadili utekelezaji wa Soko la pamoja la Jumuiya ya Afrika  Mashariki (Common Market Protocol 2010)  tangu ilipoanzishwa upya mwaka 2010.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...