Na Bakari Madjeshi,Globu ya Jamii
Taasisi ya
Sekta Binafsi nchini (TPSF) imekutana na wadau wake kujadili utekelezaji wa
Soko la pamoja la Jumuiya ya Afrika Mashariki
(Common Market Protocol 2010) tangu
ilipoanzishwa upya mwaka 2010.
Wanachama wa
Jumuiya hiyo walingia makubaliano ya pamoja ili kuongeza utengamano ambao
ulilenga zaidi kuongeza uhuru wa watu kupita nchi za Afrika Mashariki, Kuongeza
uhuru wa kusafirisha Mizigo na Biashara pamoja Uhuru wa Mitaji (Free Movement
of Capital).
Akizungumza
na Waandishi wa Habari katika majadiliano hayo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi
wa Sera – Taasisi ya Sekta Binafsi, Gilead Teri amesema kuwa wamekutana kufanya
tathmini kujua changamoto pamoja na uboreshaji katika soko hilo.
Amesema
wamekutana kujadili ili baadae kutoa
maoni kwa Serikali pamoja na viongozi wa Jumuiya hiyo, pia ni jinsi gani
Tanzania inaweza kunufaika zaidi na soko la pamoja.
Katika soko
hilo Tanzania inanufaika zaidi kupata Kodi,Wananchi kupata ajira kutokana na
soko kubwa, familia kupata kipato pamoja na kukua kwa Teknolojia ya uzalishaji.
Sehemu ya Wadau wa Taasisi ya Sekta
Binafsi wakifuatilia mada iliyokuwa ikiwasilishwa na Mkurugenzi wa Sera wa
TPSF, Gilead Teri.
Mkurugenzi wa Sera –
Taasisi ya Sekta
Binafsi, Gilead Teri akizungumza na baadhi ya wadau wa Taasisi hiyo juu
ya
kujadili utekelezaji wa Soko la pamoja la Jumuiya ya Afrika Mashariki
(Common Market Protocol 2010) tangu ilipoanzishwa upya mwaka 2010.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...