Asasi ya Kibunge inayojihusisha na masuala ya
Idadi ya watu na maendeleo (TPAPD) imeelezea umuhimu wa kuweka kipaumbele
kwenye masuala ya uzazi wa mpango ili kukabiliana na ongezeko la kasi la idadi
ya watu ambayo kwa sasa ni wa asilimia 2.7 kwa mwaka.
Tamko la TPAPD lilitolewa leo katika kuadhimisha siku ya
Kimataifa ya Wanawake Machi 8, limesema matumizi ya njia za uzazi wa mpango
yanaweza kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi (MMR) kwa asilimia 44, na
kupunguza vifo vya watoto kwa asilimia 35. Vifo vya wanawake katika uzazi
vimefikia 556 kwa kila vizazi hai 100,000 mwaka 2015 kutoka vifo 454 katika
kila vizazi hai mwaka 2010.
TPAPD chini ya Mwenyekiti wake Mhe Dkt Mary Mwanjelwa
iliamua kutoa tamko hili hivi karibuni katika kikao cha kamati tendaji mjini
Dar es Salaam kilichojadili umuhimu wa uzazi wa mpango katika harakati za
kujenga Tanzania ya uchumi wa kati na uchumi wa viwanda.
Tamko hilo lililotiwa saini na Mwenyekiti Dkt Mwanjelwa
limesema:
“uzazi wa mpango unahitajika katika kuiwezesha nchi
kukabiliana na ongezeko la kasi la idadi ya watu inayochangiwa na uzazi wa
kiwango cha wastani wa watoto sita kwa kila mwanamke aliye katika umri wa
uzazi. Hali hii huchangia utegemezi pamoja na umaskini; na pia hudumaza juhudi
za taifa za kufikia malengo ya maendeleo”.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...