Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii 

MAOMBI kwa ajili ya Taifa yamefanyika leo Jijini Dar es salaam na kuhudhuriwa na Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga pamoja na Mchungaji maarufu na mfanya biashara na mwanzilishi wa Huduma ya Bill Winston, Bill Winston kutoka nchini Marekani.

Mkutano huo uliokuwa na lengo la kuliombea taifa uliweza kuhudhuriwa na viongozi wa dini na serikali na Bishop kutoka nchini Zambia Bernard Nwaka aliendesha maombi hayo. 

Aliyewahi kuwa Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia kanda ya Afrika Dr Oby Ezekwesili aliweza pia kuchangia mada juu ya kuliombea taifa na namna wananchi wanavyotakiwa kuishi ndani ya nchi yao.
Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustino Mahiga akzungumza katika mkutano wa maombi ujulikanao kama Tanzania National Prayer uliofanyika leo Jijini Dar es salaam na kuendeshwa na Mchungaji maarufu na mfanya biashara na mwanzilishi wa Huduma ya Bill Winston, Bill Winston. 
Mchungaji maarufu na mfanya biashara na mwanzilishi wa Huduma ya Bill Winston, Bill Winston akizungumza na wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa maombi kwa taifa ujulikanao kama Tanzania National Prayer uliofanyika leo Jijini.
Aliyewahi kuwa Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia kanda ya Afrika Dr Oby Ezekwesili akizungumza na wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa maombi kwa taifa ujulikanao kama Tanzania Natipnal Prayer uliofanyika leo Jijini.
Bishop Bernard Nwaka kutoka Zambia akiongoza maombi kwa ajili ya taifa yaliyofanyika leo Jijini Dar es salaam na kuhudhuriwa na Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Augustino Mahiga,Mchungaji maarufu na mfanya biashara na mwanzilishi wa Huduma ya Bill Winston, Bill Winston na Aliyewahi kuwa makamu wa raisi wa benki ya Dunia kanda ya Afrika Dr Oby Ezekwesili.
.Picha zote na Zainab Nyamka.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...