Rais Mstaafu Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete leo amekutana na Balozi wa Canada nchini Mhe. Ian Myles aliyemtembelea ofisini kwake Masaki jijini Dar es Salaam.
Mheshimiwa Balozi Ian Myles aliwasilisha ujumbe maalum kutoka kwa Mheshimiwa Lloyd Axworthy, Mwenyekiti wa Global Refugee Initiative na Waziri Mstaafu wa Mambo ya Nje wa Canada.
Mheshimiwa Rais Mstaafu amepokea ujumbe huo na kufanya mazungumzo na Balozi huyo wa Canada nchini kuhusu shughuli zake baada ya kustaafu hususan ushiriki wake katika Kamisheni ya Elimu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...