Mkuu wa Wizara ya Paspoti
za Ndani na Shirika la Uandikishaji wa Raia wa Jamhuri ya Sudan, Luteni
Jenerali Awad Al Neil Dahia, (katikati) akikabidhi hedaya kwa Kaimu Kamishna
Jenerali wa Uhamiaji, Hannelore M. Manyanga,
baada ya kikao ambacho Maafisa Uhamiaji toka Vitengo vya TEHEMA na
Udhibiti wa Mipaka waliwasilisha mbinu anuai za kudhibiti Wahamiaji.
Naibu Kamishna wa Uhamiaji,
Fulgence Mutarasha, Mfawidhi wa Kituo cha Uhamiaji Uwanja wa Ndege Mwl. JK
Nyerere akitoa maelezo ya Utendaji wa Shughuli za Kiuhamiaji kwa mgeni wake, Mkuu
wa Wizara ya Paspoti za Ndani na Shirika la Uandikishaji wa Raia wa Jamhuri ya
Sudan, Luteni Jenerali Awad Al Neil Dahia, (katikati) ambaye alisindikizwa na Maafisa toka Wizara ya
Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki pamoja na Shirika la Uhamiaji
la Kimataifa, IOM, Tanzania.
1.
Mkuu wa Wizara ya Paspoti
za Ndani na Shirika la Uandikishaji wa Raia wa Jamhuri ya Sudan, Luteni
Jenerali Awad Al Neil Dahia, (katikati) akipitishwa eneo la Kuwasili Abilia ndani ya
Uwanja wa Ndege Mwl. J.K Nyerere alipotembelea Kituo cha Uhamiaji uwanjani
hapo kujifunza shughuli za Uhamiaji
Tanzania.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...