Na Scholastica Njozi – Law School of Tanzania

Waziri wa Katiba na Sheria, Prof. Palamagamba Kabudi amewataka watumishi wa Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (Law School) kutambua kuwa wamebeba dhamana kubwa kwa Taifa. 

Waziri Kabudi ametoa wito huo leo alipotembelea Taasisi hiyo wakati akiwa katika ziara ya kutembela taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo ili kujionea  namna Taasisi hiyo inavyotoa mafunzo.

“Nataka niwahakikishie kuwa mmebeba jukumu kubwa sana kwa Taifa hivyo mnapotekeleza majukumu yenu zingatieni sana kuhakikisha wahitimu wanakuwa na maadili, wasiopenda rushwa na kubwa zaidi watambue wanakwenda kuwatumikia watanzania maskini”, alisema Mhe. Waziri.”  Prof. Kabudi aliongozana na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Amon Mpanju.

Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa Taasisi Dkt. Zakayo Lukumay, amesema watahakikisha wahitimu wote wanakuwa na uzalendo kwa nchi yao kwa kupitia mafunzo wanayoyapata. 
Prof. Palamagamba Kabudi mwenye tai nyekundu akiwa na viongozi wa Taasisi alipotembelea majengo.
Prof. Palamagamba Kabudi, akimsaidia mwanafunzi  Bi. Jesca Mbawala namna ya kutafuta vitabu kupitia mtandao, alipotembelea maktaba ya Taasisi.

Waziri wa Katiba na Sheria, Prof.Palamagamba Kabudi akitia saini kitabu cha wageni

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...