Efm redio inatarajia kuzima kiki zote kwa kuwasha muziki wilaya ya Kigamboni, siku ya Jumamosi ya tarehe 9/9/2017 katika Bar ya G5 ikiwa ni muendelezo wa tamasha la Mziki Mnene lililoanza wiki mbili zilizopita ambapo burudani ya muziki kutoka kwa RDJs wa EFM na wasanii mbalimbali akiwemo Sholo Mwamba, Yuda msaliti, Daina Nyange, Timbulo na wengine wengi watakiamsha katika Bar hiyo.

Na katika kuipa kipaumbele michezo, na kuinua vipaji vya vijana katika uimbaji, Efm itatafuta vipaji vya muziki wa Singeli “Singeli Michano” katika Kiwanja cha Machava ambapo mshindi katika kila wilaya atapata fursa ya kurekodi nyimbo bure, Ikifuatiwa na mechi ya kirafiki kuanzia saa 10:00 Jioni baina ya timu ya EFM na KOC Veterans katika uwanja wa Kibugumo –Kigamboni na Asubuhi Efm jogging itajumuika na jogging club za Kigamboni kukata wese na kuweka mwili fresh kwa mbio za mwendo pole.

Vilevile wakazi wa Kigamboni watapata nafasi ya kujumuika, kujadili mambo kadha wa kadha na watangazaji mahiri wa kipindi cha Joto la Asubuhi, Sports Headquarters, Uhondo, na Ladha 3600 katika kiwanja cha MACHAVA siku ya Ijumaa tarehe 8/9/2017 kuanzia saa 12:00 asubuhi hadi saa 9:00 Alasiri ambapo vipindi hivyo vitarushwa live kutoka uwanjani hapo.
Efm mziki mnene, zima kiki washa muziki.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...