Na Tiganya Vincent
Sikonge

SERIKALI ya Mkoa wa Tabora imeiagiza Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge kutolipa malipo ya kiasi cha zaidi ya milioni 300 kwa ajili ya miradi miwili ya maendeleo ambayo imebainika kuwa na kasoro mbalimbali.
Agizo hilo limetolewa jana mjini Sikonge na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri baada ya kutembelea mradi wa ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Kikungi Kata ya Chabutwa na ujenzi wa barabara ya lami mjini Sikonge.
Alisema katika mradi wa Zahanati  maelezo Uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge yanaonyesha kuwa mjenzi wa Zahanati huo amekiuka makubaliano ya mpango wa ujenzi na vifaa vitakavyotumika katika (BOQ).
Mwanri alisema kuwa mjenzi wa Zahanati hiyo amekuwa akitumia vifaa zaidi au pungufu na wakati mwingine ametumia vifaa katika ujenzi wa majengo ya ZAhanati hiyo ambavyo havikuonyeshwa katika BOQ bila makubaliano na Halmashauri hiyo.
Kwa mujibu wa makubaliano mradi huo wa Zahanati unapaswa kugharimu shilingi milioni 170 ikiwa ni gharama za vifaa shilingi milioni 130 na gharama za mjenzi milioni 40 lakini kwa sababu ya mjenzi wake kutofuata maelezo ya BOQ zinaweza kuzidi.
Katika mradi wa pili ambao ni ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami kwa urefu kilometa moja kwa gharama za shilingi milioni 220.
Mkuu huyo wa Mkoa alisema mradi huo unaonekana kujengwa chini ya kiwango na muda ambao mkandarasi alipaswa ameameashamaliza umeshapita.
Kufuatia kasoro hizo katika miradi hiyo miwili Mkuu huyo wa Mkoa amemwagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Sikonge kutoidhinisha malipo ambayo yalikuwa hayajafanyika kwa mjenzi wa Zahanati ya Kikungi ya shilingi milioni 170 na yale yaliyokuwa yamebaki ya zaidi shilingi milioni 70 zilizokuwa zimebaki kwa mradi wa barabara.
Alisema kuwa wajenzi wote wa miradi hiyo watalipwa baada ya timu ya wataalamu kutoka Mkaguzi wa Hesabu Serikali za Mitaa  Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Ofisi ya Wakala wa Barabara Tanzania mkoa wa Tabora, Taasisi ya Kupambana na kudhibiti Rushwa(PCCB) na Wakala wa Majengo Tanzania(TBA).
Mwanri alisema timu hiyo inalenga kutafuta ukweli kama taratibu za kutoa zabuni kwa wajenzi zilifuatwa na ikiwa vifaa vilivyotumika vinalingana na thamani halisi ya fedha na makubaliano katika BOQ.
Kwa upande wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Sikonge Simon Ngatunga alisema kuwa alisema katika mradi wa Zahanati mjenzi aliamua kutumia baadhi ya vifaa hata ambavyo havimo katika BOQ bila hata kuijulisha Ofisi yake.
Alisema kuwa katika mradi wa barabara licha ya kutokwisha unaonyesha kuwa uko chini ya kiwango na kumshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kuunda timu ya wataalamu kuchunguza miradi hiyo ili waone kama iko katika kiwango.
Ngatunga alisisitiza kuwa hawezi kulipa hadi hapo timu ya wataalamu hapo itakapomuhakikishia kuwa taratibu zote zimezingatiwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...