Na Mathias Canal, Dar es salaam
Mkurugenzi
Mkuu wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa, (FAO), José Graziano
da Silva, leo Jumanne Septemba 5, 2017 amefanya mazungumzo na waziri wa kilimo
Mifugo na Uvuvi Mhe Dkt Charles Tzeba ikiwa ni mwanzo wa ziara yake ya kikazi
nchini Tanzania.
Katika
ziara hiyo Bw. Graziano da Silva atafanya mazungumzo na viongozi waandamizi wa
Serikali, wadau na anatarajiwa kukutana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar,
Dkt. Ali Mohamed Shein sambamba na Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi
wa Zanzibar, Hamad Rashid Mohamed.
Ziara hii
ya Mkurugenzi Mkuu inajili wakati FAO ikiadhimisha miaka 40 toka kuanza
shughuli zake hapa Tanzania Hafla ambayo itahudhuriwa na Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bi. Samia Suluhu Hassan.
Katika
mazungumzo na Waziri wa Kilimo Mifugo na Uvuvi, Mkurugenzi Mkuu wa FAO anabadilishana
mawazo na Serikali ya Muungano wa Tanzania kwenye masuala makuu yanayohusiana
na uhakika wa chakula na maendeleo ya kilimo, ikijumuisha juhudi za FAO kitaifa
na kikanda.
Pia
yamejadiliwa mambo mengine yanayohusiana na ushirikiano kati ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania na FAO, pia masuala ya umuhimu kati ya pande hizo mbili.Mbali ya
Maafisa wa Serikali, Mkurugenzi Mkuu atakutana na wadau wengine wa FAO hapa
nchini wakiwa ni pamoja na asasi za kiraia, taasisi za elimu, na taasisi za
utafiti.
Mkurugenzi
Mkuu wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa, (FAO), José Graziano
da Silva (Kulia), akimpongeza Waziri wa kilimo
Mifugo na Uvuvi Mhe Dkt Charles Tzeba mara baada ya kuelezea taarifa mbalimbali zihusuzo wizara hiyo. leo Jumanne Septemba 5, 2017.
Waziri wa kilimo
Mifugo na Uvuvi Mhe Dkt Charles Tzeba akizungumza kabla ya kumkaribisha Mkurugenzi
Mkuu wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa, (FAO), José Graziano
da Silva, kuzungumzia ujio wake nchini na ushirikiano baina ya FAO na serikali ya Tanzania. leo Jumanne Septemba 5, 2017.
Mkurugenzi
Mkuu wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa, (FAO), José Graziano
da Silva, akizungumzia na wataalamu mbalimbali katika Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi juu ya ujio wake nchini na ushirikiano baina ya FAO na serikali ya Tanzania. Kulia kwake ni Waziri wa kilimo
Mifugo na Uvuvi Mhe Dkt Charles Tzeba. leo Jumanne Septemba 5, 2017.
Waziri wa kilimo
Mifugo na Uvuvi Mhe Dkt Charles Tzeba akipokea simu 50 kutoka kwa Mkurugenzi
Mkuu wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa, (FAO), José
Graziano
da Silvakwa ajili ya wataalamu wa kilimo kuzitumia kukusanya taarifa mbalimbali na kuziwasilisha kwa jamii. leo Jumanne Septemba 5, 2017.
Waziri wa kilimo
Mifugo na Uvuvi Mhe Dkt Charles Tzeba akionyesha moja ya siku kati ya 15 alizokabidhiwa na Mkurugenzi
Mkuu wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa, (FAO), José
Graziano
da Silva kwa ajili ya wataalamu wa kilimo kuzitumia kukusanya taarifa mbalimbali na kuziwasilisha kwa jamii. leo Jumanne Septemba 5, 2017.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...