ZIKIWA zimebaki siku chache tu kufanyika kwa mbio za Rock City Marathon, kampuni ya Ujenzi ya CRJE leo imekabidhi hundi yenye thamani Tsh milioni 10 kwa waandaaji wa mbio hizo ikiwa ni udhamini wa kampuni hiyo.
Mbio zinazotarajiwa kufanyika Octoba 29 mwaka huu, Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Akikabidhi hundi hiyo kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya mbio hizo Bw Zenno Ngowi, Ofisa Mahusiano na Utawala wa kampuni ya CRJE Bw Henry Kasapira alisema udhamini huo unalenga kuunga mkono juhudi za serikali kuhamasisha michezo na utalii wa ndani hapa nchini.
“Michezo huleta uimara wa afya na uimara wa afya ndio nguzo muhimu katika sekta ya ujenzi na ndio maana pamoja na kuinua utalii tunaunga mkono pia mpango huu unaolenga kuhamasisha uimara wa afya za wananchi.’’ Alisema.
Aliahidi kuwa kampuni yake itaendelea kushirikiana na waandaaji wa mbio hizo katika kuboresha zaidi mbio hizo kwa miaka ijayo huku akitoa wito kwa vijana wengi zaidi kutoka mikoa mbalimbali kujiandaa kwa ajili ya mbio hizo.
Akizungumza baada ya kupokea hundi hiyo, Ngowi alisema ushiriki wa kampuni hiyo ya kimataifa katika kufanisha Rock City Marathon utaongeza viwango vya ubora wa mbio hizo sambamba na kuwavutia zaidi washiri wa kamataifa ambao wamekuwa wakiiamini kampuni kutokana na utendaji wake wenye ufanisi.
Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Ujenzi ya CRJE (East Africa Ltd), Bw Xie Zhixiang (kushoto) akikabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya sh milioni 10 kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya mbio za Rock City Marathon Bw Zenno Ngowi (kulia) ikiwa ni udhamini wa mbio hizo wakati wa hafla fupi ya makabidhiano iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo. Wengine ni pamoja na Mahusiano na Utawala wa kampuni ya CRJE Bw Henry Kasapira (wa pili kushoto) na Mratibu wa mbio hizo kutoka kampuni ya Capital Plus International (CPI), Bw. Steven Otieno
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...