1.LESENI YA MAKAZI
NININI.
Leseni ya makazi
ni leseni/kibali maalum kinachotolewa kwa
mmiliki wa makazi
ili kutambua na
kurasimisha makazi hayo.
Leseni ya
makazi ni nyaraka
ya umiliki wa
makazi kama ilivyo
nyaraka nyingine za umiliki
wa ardhi. Leseni
ya makazi ni
kwa ajili ya
ardhi makazi tu
na si ardhi
nyingineyo.
2. JE
LESENI ZA MAKAZI
ZINATAMBULIWA NA SHERIA.
Ndio, leseni za makazi
ni kwa mujibu
wa sheria namba
4/1999 Sheria ya Ardhi.
Leseni za makazi
zinatambuliwa na kifungu
cha 23 cha
sheria hiyo.
Kwahiyo
wanaodhani kuwa leseni
za makazi ni
mpango tu wa
serikali za mitaa
na watendaji wa
kata wajue sio
kweli. Leseni za
makazi ni nyaraka
iliyo kisheria kwa
mujibu wa kifungu
hicho japo juu.
3. TOFAUTI
YA LESENI YA
MAKAZI NA HATI .
Hati ni “Right Of Occupancy”
kwa jina la
kitaalam, wakati leseni
ya makazi ni “Derivative Right”
. Tofauti za
viwili hivi ni
nyingi ila kubwa ya
kukufanya uelewe ni
kuwa, leseni ya makazi
hutolewa kwa makazi ya mjini
ambayo hayajapimwa na
hayakuwa rasmi lakini
yasiyo hatarishi.
Wakati hati
hutolewa katika makazi
rasmi na ambayo
yamepimwa. Isipokuwa la
kuzingatia ni kuwa
iwe leseni ya makazi
ama hati vyote
vinatambuliwa na serikali kama
nyaraka rasmi za
umiliki na kila
moja ina haki
sawa na nyingine katika
umiliki.
KUSOMA
ZAIDI sheriayakub.blogspot.com
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...