Na  Bashir  Yakub.

1.LESENI  YA MAKAZI  NININI.

Leseni  ya  makazi  ni  leseni/kibali  maalum kinachotolewa  kwa  mmiliki  wa  makazi  ili  kutambua  na  kurasimisha  makazi  hayo.
 Leseni  ya  makazi  ni  nyaraka  ya  umiliki  wa  makazi   kama  ilivyo  nyaraka  nyingine za  umiliki  wa  ardhi.  Leseni  ya  makazi  ni  kwa  ajili  ya  ardhi  makazi  tu  na  si  ardhi  nyingineyo.

2.  JE  LESENI  ZA  MAKAZI  ZINATAMBULIWA  NA  SHERIA.

Ndio, leseni  za  makazi  ni  kwa  mujibu  wa  sheria  namba  4/1999 Sheria  ya  Ardhi.  Leseni  za  makazi  zinatambuliwa  na  kifungu  cha  23  cha  sheria  hiyo. 

Kwahiyo  wanaodhani  kuwa  leseni  za  makazi  ni  mpango  tu  wa  serikali  za  mitaa  na  watendaji  wa  kata  wajue  sio  kweli.  Leseni  za  makazi  ni  nyaraka   iliyo  kisheria  kwa  mujibu  wa  kifungu  hicho  japo  juu.

3.  TOFAUTI  YA  LESENI  YA  MAKAZI  NA  HATI .

Hati ni “Right  Of  Occupancy”  kwa  jina  la  kitaalam,  wakati  leseni  ya makazi ni  “Derivative Right” .  Tofauti  za  viwili  hivi  ni  nyingi  ila kubwa  ya  kukufanya  uelewe  ni  kuwa,  leseni  ya makazi  hutolewa kwa  makazi  ya mjini  ambayo  hayajapimwa  na  hayakuwa   rasmi  lakini  yasiyo  hatarishi.

Wakati hati  hutolewa  katika  makazi  rasmi  na  ambayo  yamepimwa.  Isipokuwa  la  kuzingatia  ni  kuwa   iwe  leseni  ya makazi  ama  hati  vyote  vinatambuliwa  na serikali  kama  nyaraka  rasmi  za  umiliki  na  kila  moja  ina  haki  sawa na  nyingine  katika  umiliki.
                   
 KUSOMA  ZAIDI  sheriayakub.blogspot.com


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...