Na: Frank Shija – MAELEZO

Chama cha Wahasibu Tanzania (TAA) kimeanzisha huduma ya Dawati la Mhasibu itayaofanyika kwa mara ya kwanza tarehe 07 Oktoba 2017 kuanzia saa 3: 00 asubuhi katika viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es Salaaam.

Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa Chama hicho Dkt. Fred Msemwa alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kuhusiana na huduma hiyo leo jijini Dar es Salaam.

Dkt. Msemwa amesema kuwa kupitia Dawati hilo wahasibu, wataalam wa kodi, fedha na biashara watajumuika pamoja na kukutana na wananchi wa kawaida, wafanyabiashara wadogo na wakubwa na kuwapatia huduma bure.

“Kupitia Dawati hili la Mhasibu litatukutanisha na wadau wengine wa masuala ya biashara na ujasiriamali hili kwa pamoja tuweze kutoa huduma za mbalimbali za kijasiriamali zianazohusisha masuala ya mahesabu bila ya malipo” alisema Dkt. Msemwa.
Mwenyekiti wa Chama cha Wahasibu Tanzania (TAA) Dkt. Fred Msemwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu huduma ya Dawati la Mhasibu itakayofanyika tarehe 07 Oktoba 2017 katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Chama hicho Dyoya James Dyoya na Afisa Mtendaji Mkuu wa TAA Bw. Patrice Sigungu.
Katibu Mkuu wa Chama cha Wahasibu Tanzania (TAA) Dyoya James Dyoya (kushoto) akielezea jambo mbele ya waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu huduma ya Dawati la Mhasibu itakayofanyika tarehe 07 Oktoba 2017 katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo. Kutoka kulia ni Afisa Mtendaji Mkuu wa TAA Bw. Patrice Sigungu na Mweneyekiti wa chama hicho Dkt. Fred Msemwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...