Na Mwandishi Wetu Tarime- Mara.
Waziri
wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu
ametoa miezi sita kwa Wakuu wa Shule za Msingi na Sekondari nchini
kuanzisha Madawati ya Ulinzi na Usalama wa Watoto kwa ajili ya
kusikilizamatatizo ya wanafunzi hasa wanafunzi wa kike.
Akizungumza
wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Mtoto wa KikeKitaifa
iliyofanyika katika wilaya ya Tarime mkoani Maraamewasisitiza wakuu wa
shule za Msingi na Sekondari kuzingatia uwepo wa dawati la ulinzi na
usalama wa mtoto kike katika shule zao ili kuwa salama na kuwa na
mahali pa keleza matatizo yao.
Mhe.
Ummy ameongeza kuwa suala la kumlinda mtoto wa kike ni jukumu la kila
moja katika jamii na kuwapongeza wadau wa maendeleo ya watoto kwa
jitihada zao na kushirikiana na Serikali kutoa elimu kwa wanajamii
kuhusu madhara ya mimba za utotoni, ukeketaji na ukatili dhidi ya
wanawake na watoto.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akizindua kampeni ya kitaifa ya kutokomeza mimba za utotoni yenye kauli mbiu isemayo:” "Najitambua Elimu ndio Mpango mzima".
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akibonyeza kitufe kuzindua ujumbe wa radio wa kampeni ya kutokomeza mimba za utotoni yenye kauli mbiu isemayo:” Najitambua Elimu ndio Mpango Mzima”
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watoto, wadau na madereva bodaboda wa Wilaya ya Tarime mkoani Mara muda mfupi baada ya Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Kike yaliyofanyika kitaifa wilayani Tarime mkoani Mara. Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini WAMJW.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...