Na Mathias Canal, Mbeya
Naibu
Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa Jana Novemba 29, 2017
amemuagiza Mkurugenzi Wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya kumsimamisha
kazi Afisa Kilimo Wilaya ya Mbeya anayesimamia zao la Pareto Ndg
Emmanuel Halinga ili kupisha uchunguzi.
Mhe
Naibu Waziri ametoa agizo hilo wakati wa Mkutano wa hadhara uliofanyika
katika Kijiji cha Jojo Kata ya Santilya akiwa kwenye ziara ya kikazi
Katika Mikoa ya Nyanda za Juu kusini mwa Tanzania mara baada ya Mhe
Mbunge wa Jimbo hilo Mhe Oran Njeza na Wananchi wote waliokuwepo kwenye
mkutano huo wa hadhara kumrushia shutuma nzito na kumkataa mtaalamu huyo
wa kilimo mbele ya Naibu Waziri.
Alisema
kuwa pamoja na zao hilo la Pareto kuwa la kwanza kwa uzalishaji katika
nchi za Afrika huku likiwa zao la pili kwa uzalishaji Duniani lakini
bado halijamkomboa Mkulima nchini jambo ambalo linaonyesha namna ambavyo
baadhi ya wataalamu Wa Kilimo wameshindwa kutekeleza majukumu yao
ipasavyo.
Alisema
kuwa wataalamu wa kilimo walipaswa kusimamia kwa kiasi kikubwa zao hilo
kwani Pato lake ni wastani wa tani 2000 kwa mwaka sawa na Bilioni 12
mpaka 14 ambapo katika kipindi hili bei ya kuanzia Mkulima analipwa
shilingi 2300 kwa kilo lakini inapanda mpaka shilingi 3300 kulingana na
ubora wa zao hilo ambalo mkulima amelima.
Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akizungumza wakati wa Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Jojo Kata ya Santilya akiwa kwenye ziara ya kikazi Katika Mikoa ya Nyanda za Juu kusini Kwa Tanzania, Jana Novemba 29, 2017. Picha zote Na Mathias Canal
Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akisisitiza jambo wakati wa Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Jojo Kata ya Santilya akiwa kwenye ziara ya kikazi Katika Mikoa ya Nyanda za Juu kusini Kwa Tanzania, Jana Novemba 29, 2017.
Naibu Waziri Wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akizungumza wakati wa Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Jojo Kata ya Santilya akiwa kwenye ziara ya kikazi Katika Mikoa ya Nyanda za Juu kusini Kwa Tanzania, Jana Novemba 29, 2017.
Mbunge wa Jimbo la Mbeya Vijijini Mhe Oran Njeza akizungumza katika mkutano huo kufikisha kilio cha wananchi mbele ya Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwwa kuhusu zao la Pareto na matatizo la wafanyabiashara kujaza Lumbesa kwenye uuzaji wa mazao mbalimbali likiwemo zao la viazi wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika Kijijini Jojo Kata ya Santilya, Jana Novemba 29, 2017.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...