Na Agness Francis,Blog ya Jamii.
MCHEZO kati ya Timu ya Azam FC dhidi ya Timu ya Yanga unaotarajiwa kuchezwa Jumamosi saa 1 usiku kwenye Uwanja wa Azam Complex, Timu ya Azam imesema kuwa Timu imeishaingia Kambini kwaajili ya maandalizi ya mchezo huo.
Akizungumzia kuelekea kuhusu mchezo huo Afisa Habari wa Azam FC, Jaffary Iddy Maganga amesema kuwa kikosi cha Azam FC iko imara katika kuweza kuwakabili Yanga na matokeo ya mchezo huo ni Dakika 90.
Azam watashuka dimba ni siku hiyo dhidi ya YangAfricans mchezo utakaokuwa wa kukata na shoka ambapo timu zote mbili zitakuwa na hamu ya kupata Ushindi wa pointi Tatu siku hiyo.
"Baada ya Timu kurejea kutokea Jijini Mbeya ambapo tulikokuwa na mchezo wetu na Tanzania Persons jana imeingia kambini na kuanza mazoezi kwa ajili ya maandalizi dhidi ya YangAfrica. Mchezo huo utakuwa ni mgumu ukizingatia Yanga nayo ni timu nzuri na Ina kikosi kipana lakini na sisi tumejipanga kunyakua pointi Tatu zenye ushindi wa mabao" Amesema Maganga
Mpaka sasa hivi Azam FC anashika nafasi ya pili kwa kwa pointi 30 kwenye misimamo Tanzania Bara akifatiwa na mabingwa watetezi YangAfrica mwenye pointi 25, huku wakiingozwa na pointi 33 za timu ya Simba.
Afisa Habari wa AzamFc, Jafari Iddy Maganga akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya timu kuanza rasmi jana mazoezi kule Chamazi Complex, leo katika ofisi zao zilizopo Mzizima Jijini Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...