Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani anayehudumia pia Austria, Balozi Abdallah Possi akiwasili katika Ikulu ya Viena, nchini Austria kwa kujitambulisha rasmi kwa Rais wa nchi hiyo, Dkt. Alexander Van der Bellen. Ubalozi wa Tanzania nchini Ujerumani unahudumia pia Austria, miongoni mwa maeneo yake ya uwakilishi.
Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani anayehudumia pia Austria, Balozi Abdallah Possi akiwasilisha hati ya utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Austria, Dkt. Alexander Van der Bellen katika hafla fupi ya kujitambulisha iliyofanyika Ikulu ya nchi hiyo, leo.
Rais wa Jamhuri ya Austria, Dkt. Alexander Van der Bellen akizungumza jambo na Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani anayehudumia pia Austria, Balozi Abdallah Possi, aliyefika Ikulu hapo kujitambulisha.
Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani anayehudumia pia Austria, Balozi Abdallah Possi akiwa katika picha ya pamoja na Rais wa Jamhuri ya Austria, Dkt. Alexander Van der Bellen.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...