Frank Mvungi- MAELEZO, Dodoma.
Vyombo vya Habari nchini vimeaswa kuunga mkono juhudi za Serikali katika utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo kwa maslahi mapana ya Taifa.
Akizungumza Wakati wa ziara yake yakutembelea Vyombo vya habari leo mjini Dodoma Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi amesema kuwa dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano ni kuhakikisha kuwa wananchi wanapata maendeleo endelevu kwa kuwa misingi ya Taifa letu imejengwa katika uchumi jumuishi.

“ Kuna umuhimu kwa vyombo vya habari kushiriki kikamilifu kueleza faida za miradi mikubwa ya maendeleo inayotekelezwa kama ule wa ujenzi wa reli ya Kisasa (Standard Gauge) kwa wananchi ili nao washiriki kikamilifu katika utekelezaji wake ambapo ukishakamilika utakuwa kichocheo kikubwa cha maendeleo” Alisisitza Dkt. Abbasi.

Akifafanua amesema kuwa dhamira yakuwaletea wananchi maendeleo inaendelea kutekelezwa kupitia mfumo wa elimu bure, uzalishaji wa umeme wakutosha, Ujenzi wa uchumi wa Viwanda, ujenzi wa miundo mbinu kama barabara, reli na upatikanaji wa huduma muhimu kama madawa ambapo Serikali imeongeza bajeti ili kuhakiksha kuwa kila mwananchi anapata huduma muhimu na za msingi katika ubora unaotakiwa.
 Mkurugenzi wa ABM Fm Bw. Abdallah Majura (Mwenyeshati Jeupe) akimuonesha Mkurugenzi wa Idara ya Habari-MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi Chumba cha kurushia matangazo wakati wa ziara yake ikiwa ni sehemu ya utaratibu wake wa kutembelea vyombo vya habari ili kuona utendaji kazi wa vyombo hivyo leo Mjini Dodoma. Mkurugenzi wa Idara ya Habari-MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi akimsikiliza Mkurugenzi wa ABM Fm Bw. Abdalah Majura (Mwenyeshati Jeupe) wakati wa ziara yake yake ikiwa ni sehemu ya utaratibu wake wa kutembelea vyombo vya habari ili kuona utendaji kazi wa vyombo hivyo leo Mjini Dodoma.
Mkurugenzi wa Idara ya Habari-MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi akiongea na wafanyakazi wa Radio ABM FM wakati wa ziara yake yake ikiwa ni sehemu ya utaratibu wake wa kutembelea vyombo vya habari ili kuona utendaji kazi wa vyombo hivyo leo Mjini Dodoma. - Mkurugenzi wa Idara ya Habari-MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi akimkabidhi Mkurugenzi wa ABM Fm Bw. Abdalah Majura (Mwenyeshati Jeupe) toleo Maalum la Jarida la Nchi Yetu kuhusu mafaniko ya miaka miwili ya Serikali ya Awamu ya Tano. Mkurugenzi wa Idara ya Habari-MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi akifanya mahojiano maalum na Mkurugenzi wa ABM Fm Bw. Abdalah Majura (Mwenyeshati Jeupe) wakati wa ziara yake ikiwa ni sehemu ya utaratibu wake wa kutembelea vyombo vya habari ili kuona utendaji kazi wa vyombo hivyo leo Mjini Dodoma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...