Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg. John Lipesi Kayombo akiwaonyesha utekelezaji wa ilani ya CCM ya mwaka 2015 - 2020 wajumbe wa Kamati ya siasa Wilaya ya Ubungo inayoongozwa na Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya hiyo Ndg. Lucas Mgonja.

Mkurugenzi Kayombo kwa kushirikiana na watumishi wa Manispaa hiyo ameweza kujenga ukuta (fensi), vyoo na vyumba nane vya madarasa katika shule ya msingi Ubungo Plaza.

Kabla ya hapo shule hiyo ilikuwa haina uzio,hali ambayo ilikuwa ni hatarishi kwa wanafunzi wa jinsia zote.

Pia kulikuwa na uhaba wa vyoo, ambapo kilikuwa ni chanzo kikubwa cha magonjwa.Sambamba na hilo wanafunzi walikuwa wanasoma katika majengo chakavu hali iliyokuwa ikihatarisha maisha yao.

Habari njema ni kuwa Mkurugenzi Kayombo ameahidi kujenga shule ya Sekondari ya A - level katika eneo hilo.Jambo ambalo litakuwa ni Mara ya kwa Manispaa hiyo tangu ianzishwe.

Hongera Mkurugenzi Kayombo kwa kuendelea kutekeleza ilani ya CCM ya mwaka 2015 - 2020 kwa vitendo.
vyumba nane vya madarasa vikiwa katika hatua ya mwisho kabisa,katika shule ya msingi Ubungo Plaza.
 Ukuta wa shule hiyo 
 Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg. John Lipesi Kayombo akiwaonyesha utekelezaji wa ilani ya CCM ya mwaka 2015 - 2020 wajumbe wa Kamati ya siasa Wilaya ya Ubungo inayoongozwa na Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya hiyo Ndg. Lucas Mgonja.
 Vyoo vya shule hiyo vikiwa tayari kuanza kutumika.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...