Na Agness Francis Globu ya jamii.

KAMATI ya Maadili ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania(TFF) imemfungulia mashitaka Mwenyekiti wa Abajalo FC na Mjumbe wa Bodi ya Ligi Edgar Chibula kwa tuhuma ya kuikashifu na kuidhalilisha Kamati ya Bodi ya Ligi ya TFF katika vyombo vya  Habari ambapo ni kinyume na sheria. 

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam,Ofisa Habari wa TFF Clifford Ndimbo amesema kuwa  Chibura alishitakiwa Februari 28 mwaka huu kwa kosa la  kuzungumza maneno yasiofaa kwa kuidhalilisha bodi hiyo katika vyomba vya habari ikiwa ni kinyume na kufungu cha sheria  cha 50(1), (2) na (6) cha Katiba ya TFF toleo  la mwaka 2015,pia ni kinyume na sheria kanuni za maadili  toleo  la 2013.

Aidha Ndimbo amesema kwenye  shauri  hilo mtuhumiwa  huyo hakuhudhuria, isipokuwa alileta  utetezi wake kwa njia ya maandishi 
ambapo Sekretarieti ya TFF ilitoa ushahidi wa sauti(clip)  ya mahojiano aliyofanya na kituo kimoja cha redio hapa nchini. 

Ambapo kwenye mahojiano hayo mtuhumiwa alisikika akizungumza maneno hayo yasio na maadili katika maendeleo ya mpira wa miguu. 

Ndimbo amesema kutokana na utovu wa nidhamu  na kosa la kuzungumza maneno ya kuikashifu  Bodi ya Ligi ya Mpira wa Miguu TFF,  Kamati imeamua asijuhusishe na shughuli  zozote za mpira wa miguu kwa kipindi cha mwaka mmoja pamoja na faini ya Sh.milioni 3  chini ya kufungu cha  73 (4) kanuni za maadili ya TFF toleo 2013.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...