Na Agness Francis,  Globu ya Jamii. 

MWENYEKITI wa Chama cha Soka  cha Wanawake Tanzania Amina Karuma amewakumbusha viongozi  wa timu mbali mbali za soka la  wanawake  zilizoingia 8 bora katika Ligi ya  Serengeti Primer Lite  kuzingatia sheria na kanuni 17  za Mpira wa Miguu. 

Karuma amesema hayo leo jijini Dar es Salaam katika Hotel ya Chichi Kinondoni wakati wa Semina elekezi kwa viongozi hao  24  huku akiwataka watambue wajibu wao kulea wachezaji  wazuri ili kuisadia  kufikia malengo  ya kupata timu bora ya Taifa hapa nchini. 

Aidha Karuma amesema wapo karibuni kuingia kambini  na wanatarajia kucheza mechi ya kwanza na Zambia katika Kombe la Womes World ,
kabla ya kwenda kwenye challenge Cup nchini Rwanda kutetea ubingwa wao mara baada ya kuwasiliana  na Baraza la Soka la Afrika. Mashariki na Kati (CECAFA) 

Hata hivyo,  Karuma amesema licha ya wachezaji kujitahidi, ametoa mwito kwa wadhamini waendelee kujitokeza kufadhili timu hizo ili kusaidia kuleta maendeleo ya soka la wanawake  hapa nchini.Kwa upande wa Kocha Mkuu  Aliance Girls Ezekiel Chobaka amezungumzia utendaji mzuri wa timu yake tangu alipoanza rasmi kuifundisha Mei 5 mwaka jana.

"Maendeleo  ni mazuri  kwa timu yangu na ninamatumaini  kufanya vizuri  katika Ligi Kuu, vilevile tumeweza kuchukua ubingwa katika   Ligi kuu Mkoa  wa Mwanza,"  amesema Chabaka.
 Mwenyekiti wa Chama cha Soka  cha Wanawake Tanzania, Amina Karuma akizungumza na Viongozi wa Timu zilizoingia 8 bora ya Ligi ya Serengeti Primer Lite katika semina elekezi iliofanyika leo Jijini Dar es Salaam katika.
 Viongozi mbalimbali wa Timu hizo zilizoingia 8 Bora Ligi ya Wanawake Serengeti Premier Lite wakisikiliza mafunzo na maelekezo kutoka kwa Mwenyekiti wa Chama cha Soka   cha Wanawake Tanzania, Amina Karuma leo Jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...