Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Mhe. Christina Mndeme leo amekutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa dini ambapo katika kikao hicho kamati ya Amani ya Mkoa imeundwa ikihusisha viongozi wa Dini zote. Katika  kikao hicho masuala mbalimbali ya maendeleo yamejadiliwa pia, na  amewashukuru viongozi hao kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuliombea Taifa na kukemea maovu. RC Mndeme  amewaomba viongozi hao wa dini kuendelea kuliombea Taifa na pia ameahidi kuwapa ushirikaiano mkubwa kwa maendeleo ya Ruvuma na Taifa kwa ujumla pia kukemea maovu miongoni mwa jamii.
Kwa upande wao viongozi wa dini wamemshukuru mkuu wa mkoa kwa hatua hiyo waliyoiita ya kihistoria, na wameahidi kushirikiana naye pamoja na serikali bega kwa bega ili kujenga jamii yenye kujali utu, maadili na inayochukia maovu.
 Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme  Mhe. leo katika picha ya pamoja na viongozi wa dini ambao wanaunda  kamati ya Amani ya Mkoa wa Ruvuma baada ya kikao chao.
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme  Mhe. leo  akiwa na iongozi wa dini wanaounda  kamati ya Amani ya Mkoa wa Ruvuma pamoja na wadau na maafisa kutoka katika ofisi yake.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...