Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii
WAFITI
mbalimbali nchini wakiongozwa na Taasisi ya Utafiti Repoa wamekuta
jijini Dar es Salaam kwa lengo la kujadili masuala yanayohusu tafiti
huku moja ya mada ikiwa ni namna gani watakabiliana na changamoto ya
kupotoshwa kwa tafiti kutokana na kukua kwa teknolokia na hali ya
kisiasa.
Mbali
ya watafiti wa Tanzania, pia watafiti wa nchi zaidi ya 170 duniani nao
wamekutana kwenye mkutano maalumu kama ambao umefanyika nchini kujadili
masuala hayo hayo yanayohusu tafiti na changamoto zake.
Akizungumza
leo jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mkuu wa Repoa Dk.Mmari amesema
kukutana kwao kwenye mkutano huo unalenga kuzungumzia umuhimu wa taasisi
za utafiti duniani ambapo kwa mwaka huu wanazungumzia changamoto ya
ukuaji wa teknolojia na watu kupotosha tafiti kutokana na hali ya
kisiasa.
"Mkutano
huu unafanyika pia kwenye nchi nyingine 170 duniani.Moja ya ajenda ni
hii ya changamoto ya ukuaji wa teknolojia na watu kupotosha tafiti
kutoka na hali ya kisiasa.Mkutano huu unajulikana "Why thinks matter "na
umeanza saa tatu asubuhi hadi saa tano kwa nchi zote hizo,"amesema
Dk.Mmari.
Dk.
Mmari amefafanua siku hizi kuna changamoto ya mitandao ya kijamii kwani
taarifa zinasambaa kwa haraka na nyingine hazina ukweli wowote na
kusababisha viongozi kuziamini na kuzitumia katika utungaji wa sera na
kuendesha shughuli za Serikali."Hivyo imeonekana ni muhimu mwaka huu
wakazungumzia tafiti ambazo zimefanyiwa kazi kisayansi,"amefafanua
Dk.Mmari.
Ameongeza
umuhimu wa watafiti na utafiti umesaidia katika kufanya maendeleo ya
kweli ,hivyo amewahimiza Watanzania kuendelea kufanya tafiti
zitakazotumika kwa ajili ya mipango ya maendeleo ya Serikali na wadau
mbalimbali."Si vyema watafaiti wakafanya tafiti ambazo zinawekwa tu
kwenye makabati pasipo kuwa na matokeo yoyote chanya kwa Taifa,"amesema
Dk.Mmari.
Mkurugenzi Mkuu wa Tasisi ya Utafiti Nchini,REPOA, Dr Donald Mmari akizungumza wakati wa Ufunguzi wa Mkutano wa Wadau wa Tafiti Duniani ambao kwa Tanzania ulifanyika katika Ofisi za Repoa na kuitwa jina la Umuhimu wa Tafiti Duniani
Balozi wa Swideni Nchini, Katarina Rangnitt akizungumza wakati wa Mkutano wa Watafiti Duniani(WHY THINK TANKS MATTER) uliofanyika katika Taasisi ya utafiti ya Repoa kwa hapa nchini.
Mtafiti Kutoka Tasisi ya Utafiti ya Repoa, Dr Blandina Kilama akizungumza wakati wa mkutano huo wa watafiti Duniani.
Baadhi ya Maprofesa walioshiriki Mkutano huo wakiongozwa na Profesa Mwesigwa Baregu wa kwanza kulia Pichani.
Sehemu ya Wajumbe wa Mkutano huo wakisikiliza Mada Mbalimbali kutoka kwa watafiti na Wadau mbalimbali.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...