*Mkurugenzi aelezea namna wanavyotoa elimu ya kuokoa maisha ya mama mjamzito
*Wapania kumfanya mwanamke mjamzito kuwa malkia, mwanamke shujaa na mwenye thamani
*Aprili 6 mwaka huu Rais Mstaafu , Dk.Jakaya Kikwete mgeni rasmi sherehe ya miaka mitano ya uwepo wa CSI.
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii
NGUVU ya mwanamke na iheshimiwe, itukuzwe maana imeshafanya mapinduzi mengi duniani na yoyote mwenye kumdharau au kumuumiza mwanamke hafai kutambulika kama binadamu mwenye kujitambua.
Ukweli ni kwamba mwanamke ni malkia na maisha yake ya sasa na baadae yanahitaji heshima kubwa. Pamoja na hayo mheshimu mwanamke maana wewe umetoka ndani yake, na unamwita mama.
Mwanaume ili aitwe baba anahitaji mwanamke. Mwanaume mwenye akili timamu huhitaji mapenzi ya kweli na hayo hayapatikani kwingine zaidi ya kwa mwanamke. Mwanamke ni maisha.
Unaweza kujiuliza kwanini nimeanza kwa kueleza yote hayo. Kabla sijajibu sababu ya kuelezea hayo kwa kina niongeze tu mwanamke ni kiumbe mwenye thamani mbele ya viumbe vilivyopo chini ya jua .
Kwanini? Jibu ni kwamba pamoja na sababu nyingine nyingi lakini Mungu amempa kazi moja ambayo ni muhimu katika maisha ya mwanadamu. Mwanamke ndio mwenye uwezo wa kuleta mtu mpya duniani.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...