Kampuni ya isatech Water Watengenezaji wa mita za maji za kutumia LUKU kwa ajili ya matumizi mbali mbali kama Water Kiosk kwa matumizi ya community , Domestic meter kwa makazi na meter kubwa kwa ajili ya viwanda na taasisi.
Katika mazungumzo yao Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani Dkt. Abdallah Possi ameelea kufurahishwa na technolojia hiyo ambayo amesema inaweza kusaidia ukusanyaji wa mapato hususani maeneo ya vijijini ambako miundombinu ya maji bado ni tatizo.
Mhe Balozi Dr Possi ameshauri kampuni ya iSatech Water watumie fursa iliyopo na kuingia katika soko la Tanzania .
Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa iSatech water Berlin,Mr Emmanuel Mey, Balozi wa Tanzania Ujerumani Mh Balozi DKt. Abdallah Possi, Mwakilishi wa Kampuni ya iSATECH Water Tanzania Bw. Peter Kazaura na Bi. Hanna Jass kutoka iSatech water Berlin.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...