Na. Jumbe Ismailly, Hanang
MKURUGENZI Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Hanang,Mkoani Manyara,Bryceson Kibassa amepiga mafuruku walimu wa shule za msingi kuwatoza wazazi na walezi wa watoto michango ya aina yeyote ile na kuwahakikishia kwamba hakuna mtoto wa wilaya hiyo atakayetakiwa kukosa elimu kwa kisingizio cha kutolipa michango.
Mkurugenzi huyo alitoa tahadhari hiyo kwenye mkutano maalumu wa Baraza la madiwani lililokutana kupitisha mapendekezo ya makisio ya mpango na bajeti ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha wa 2018/2019 uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri hiyo.
Akifafanua kuhusu mpango wa elimu ya msingi bila malipo Kibassa alisisitiza kwamba kusiwepo na mtoto yeyote Yule wa Hanang ambaye atashindwa kwenda kusoma shule kwa kisingizio wa mchango wa aina yeyyote ile.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi huyo michango inayoruhusiwa ni ile tu ya kijamii wanayokubaliana kwa ajili ya kuboresha miundombinu bila kugusa ile michango ambayo kwenye waraka inatajwa kwamba msichangishe,isiwe kikwazo cha kuzuia mtoto yeyote kwenda shuleni.
“Tunataka watoto wote wa Hanang kwa agizo na Mheshimiwa Rais na agizo la serikali ya awamu ya tano watoto wote wawepo shuleni na kusijekuwa na mchango wa aina yeyote unaozuia mtoto wa Hanang kwenda shuleni.”alifafanua Mkurugenzi huyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...